Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

Hon. Saul Henry Amon

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

MHE. SAUL H. AMON: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia hoja zilizopo mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitangulize kutoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais kwa hatua za makusudi za kuanzisha na kulifufua Shirika la Ndege Tanzania ambalo limefanya tuwe na usafiri wa uhakika na kupunguza ajali nyingi ambazo tungepata hasa viongozi kwa kutembea kwa barabara. Vilevile kwa hatua zake za makusudi kujenga reli ya Standard Gauge pamoja na Mradi kubwa kabisa wa Umeme wa Stiegler’s Gorge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizo vilevile nataka kuongea mimi machache kwa Mheshimiwa Waziri Mpango - Waziri wetu wa Fedha na Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, biashara ina usumbufu hasa katika uingizaji wa mizigo na hili ninalizungumza na nitakuwa nalizungumza ili uweze kuliangalia. Mimi maombi yangu ni kumwomba Mheshimiwa Waziri Mpango na Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara wajaribu kuwaita wafanyabiashara wanaoingiza mizigo ndani ya nchi hii, kwa sababu hatuwezi kuzungumza kwamba sisi tunajitosheleza kwa viwanda na kuwekewa vikwazo vilivyopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kama wanasikiliza sana mimi mara nyingi Mheshimiwa Rais huwa namsikiliza sana, lakini wangesikiliza na kufuatalia kwa nini anasema punguzeni vikwazo? Amewaambia kuhusu majengo, amewaambia kwamba kodi hizi za juu mnazong’ang’ani watu hawana na ndiyo maana mnashindwa kuzikusanya. Muangalie vile alivyoondoa riba kwenye malimbikizo ya kodi watu wamelipa kiasi gani. Kwa hiyo, zile riba kubwa zikiondoka watu watalipa bila matatizo. Vilevile kuna vikwazo vingi na vikubwa sana kwenye taasisi na mamlaka mbalimbali za Serikali kwenye uingizaji wa mizigo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye uingizaji wa mizigo kutoka nje ya nchi; na ndiyo maana nimeomba viwanda na biashara pamoja na Mheshimiwa Waziri wa Fedha ukiwaita wafanyabiashara nikiwemo na mimi mwenyewe kwa sababu na-declare interest kwa sababu nafanya hizo biashara tuzungumze kwa nini watu wanakwenda porini kwa nini watu mipaka ni mingi, mikubwa na mirefu sana. Mfanyabiashara anahangaika na muda, hakuna mfanyabiashara anayehangaika na kingine, anahangaika na faida yake na muda. Sasa unapomkalisha mfanyabiashara kwanza Serikali haipati faida na mfanyabiashara hapati faida. Matokeo yake ni kwamba tunarudisha na kufifisha uchumi wa nchi nyuma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano kwa nini nazungumza kuhusu vikwazo vya biashara ambavyo vipo wakati wa uingizaji mizigo. Unakuta idara ni nyingi za Serikali zinazotoa vikwazo, TRA anakwambia mimi nimemalizana na wewe ingiza, TBS anakwambia mimi na wewe tumemalizana ingiza, anakuja mtu wa vipimo anakwambia hapana mimi kwangu hujamaliza vipimo, nianze kutumia vipimo. Hujamaliza anakuja mtu wa mionzi anakwambiwa tunataka tuangalie hizo peremende ulizoleta kuhusu mionzi. Kwa hiyo, unakuta tunarudisha nyuma sana uingizaji wa mizigo na kusababisha watu kuona kwamba ni kero kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo naomba mngekaa kama Serikali. Vilevile kama hiyo sheria ilitungwa hapa na imetengeneza vikwazo, kwa nini msiirudishe hiyo sheria hapa ili iondolewe vikwazo? Hilo nalizungumzia la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili hawa wafanyabiashara mnawatengenezea monopoly, kwa sababu haiwezekani kwamba kila mfanyabiashara atakayekwenda kununua mizigo nje ya nchi atakwenda kwenye viwanda moja kwa moja, si rahisi hata kidogo. Nitajitolea mfano mimi mwenyewe, mimi nauza vipodozi, nijitolee mwenyewe, nisimpe mtu mwingine. Vipodozi ni aina 40; nikatafute makampuni 40 waje wafanye inspection mahali niliponunulia mizigo imetoka Uingereza, Canada, Marekani, Italy na kote huko wakague? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba Serikali Tukufu, na ninaamini hata Mheshimiwa Rais angeambiwa angesema tuje tukagulie hapa hapa Tanzania. Mtu anende akanunue alete mizigo yake akaguliwe hapa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwani mnataka kuniambia kwamba kule ndiko wanajua kuangalia bora kuliko Tanzania ambayo nyie ndio mnaiona physically? Hilo ningelifanyia kazi na hilo watu wanakimbia na kunung’unika sana; hawawezi kuwaambia kwa sababu hawawezi kuwafikia, lakini mimi niliowafikia nataka mlielewe hilo mlizungumze mkae viwanda na biashara pamoja Mheshimiwa Waziri wa Fedha ili kuwarahisishia wananchi na kurahisisha ukusanyaji wa kodi. Kwa sababu mfanyabiashara hawezi kukubali, ametoka South Africa umemzua mpakani, mpaka ni mrefu ukiliangalia Ziwa Nyasa lote lile ni mpaka. Ukienda moja kwa moja Mto Songwe – Tunduma - Zambia mpaka wapi kote ni mpaka, mtu ataamua kupita mahali pengine popote ili aweze kungiza kwa sababu yeye biashara yake anataka ifanyike. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimesimama kuchangia nakuomba kwa hilo tu kwamba naomba Mheshimiwa Waziri Mpango na Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara muwaite wafanyabiasha kama alivyofanya Mheshimiwa Rais kuangalia kero za wafanyabiashara ya madini juzi ilipendeza sana mbele ya watu. watu waliongea wakaongea mpaka sasa hivi nina imani mnalifanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaamini vilevile hili mkilizungumza, mkalipeleka kwa Mheshimiwa Rais kwamba kikwazo cha watu kuingiza mizigo ndani ya nchi hii ni hiki hapa; wanavyozungumza watu wote kwamba Serikali sikivu ni kwamba Mheshimiwa Rais wetu ni msikivu kwa mambo yetu yanayotusumbua ndani ya nchi hii. Kwa hiyo, nami nimesimama kwa ajili ya hilo. Otherwise napongeza sana na ninaunga mkono Taarifa ya Kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuongea. Ahsanteni sana. (Makofi)