Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru nimepata nafasi hii ili kuzungumzia mambo yetu ya bajeti. Nampongeza Rais wangu Dkt. Magufuli kwa Ilani yake ya CCM anaboresha Tanzania yetu na kutuondoa katika umaskini wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nawapongeza Mawaziri na Mwenyekiti wa Kamati yetu ya Miundombinu na wajumbe wote. Sisi tunafanya kazi kuendana na wito wa Rais wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitazungumzia mambo machache mazito. La kwanza ni bandari. Bandari yetu Mheshimiwa Rais pamoja na Waziri wanasimamia vizuri kuanzia Dar es Salaam, Mtwara, Tanga na Zanzibar. Kwa upande wa Tanga tumepata mambo ya mafuta basi tutapata mapato zaidi na vilevile kwa Zanzibar tuboreshe bandari yetu, Muungano wetu inahusu kuboresha bandari yetu tuweze kuongeza makontena zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu Reli ya Standard Gauge. Nampongeza Mheshimiwa Rais pamoja na Waziri, sisi Kamati tumetembelea kuanzia Dar es Salaam, Morogoro kushuhudia ujenzi wa Standard Gauge. Reli hii italeta mapato kwa sababu tutaenda mpaka Mwanza na nchi za jirani kupakia mizigo na kupata fedha za kutatua matatizo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Rais na Kamati yaani Mheshimiwa Magufuli amesimamia kuleta ndege sita (6). Nia na madhumuni yake ni kuondoa umaskini katika Tanzania yetu, tunasimamia nchi yetu na wanyonge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ameleta ndege sita (6) na zinafanya kazi moja kwa moja. Hata hivyo, naomba kuboresha iende ndege China na India kuleta watalii Tanzania mpaka Zanzibar. Mungu amsaidie Mheshimiwa Rais Magufuli, Inshallah, Mungu amzidishie alete meli pia na mambo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naenda kuzungumzia barabara. Barabara yetu inafanya kazi nzuri kuanzia Dar es Salaam, Morogoro, Arusha, Mwanza. Barabara hii tukiiboresha basi italeta mapato zaidi na tutafikia uchumi wa kati. Kwa sababu unapotoka Zanzibar au nchi nyingine ile mzigo inafika mpaka nchi nyingine hivyo tutaongeza mapato na kuondoa umaskini wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu kuboresha Shirika la Posta na TTCL. Watu wa Posta najua wanafanya kazi kwa juhudi sana, amezungumza mwenzangu hapa, kwa hiyo tuongeze mishahara yao. Vilevile TTLC kuhusu mambo ya mtandao, wananchi wanapenda mitandao ya kuzungumza baina yao, basi tuwaongezee nguvu TTCL waweze kuongeza huduma hii kwa wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho kabisa, naipongeza Serikali yangu, nampongeza Rais wangu Mheshimiwa Dkt. Magufuli, nampongeza Rais wa Zanzibar, tuwe pamoja na tuongeze mambo mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu na Tanzania. Kwa hayo machache, naipongeza nchi yetu na Tanzania yetu. Ahsante sana. (Makofi)