Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

Hon. Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kusema ili Taifa lolote liweze kuendelea linahitaji viti viwili vya msingi. Taifa linahitaji uchumi shirikishi na siasa shirikishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na uchumi shirikishi. Ili uweze kuwa na uchumi shirikishi katika nchi ni lazima kuwepo na motisha ya kufanya watu wako waweze kuwa wanatafakari kwa kina na kuwa wabunifu wazuri na kutengeza mifumo ambayo itakujenga uchumi wa nchi yao. Nitolee mfano wa Bill Gates wa Marekani ameweza kukaa chini na kugundua na kutengeneza fursa za kiuchumi kwenye eneo la computer na huko akawa tajiri na akatengeza uchumi wake na akatengeza ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchumi ambao siyo shirikishi ni ule uchumi ambapo anatokea fisadi mmoja mwenye fedha zake, anakamata nchi, anaenda kwenye eneo moja tuseme la mawasiliano, anakamata zile fursa, anazuia watu wengine kuingia kwenye hizo fursa anakuwa tajiri peke yake na anakamata mpaka Ikulu. Mojawapo ya uchumi usio shirikishi ni uchumi ambao mtu anaweza akaja akachukua ardhi ya Tanzania, akachukua hati, akaenda akakopa fedha na asiendeleze, akawazuia Watanzania kutumia ile ardhi na hakuna kitu chochote ambacho Watanzania wanakipata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana utasikia wenzangu wa upande wa pili wanalalamika sana ambao wameshindwa hata kutumia milioni 400, sielewi kwa nini tunahangaika na watu kama hao kusikiliza ushauri wao. Ndiyo maana Mheshimiwa Lema leo kwa mara ya kwanza pamoja na kujua migogoro ya ardhi iliyopo kwenye Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha amesimama hapa anapinga watu kunyang’anywa ardhi na Wizara ya Ardhi. Anakataa kwa sababu anajua kwamba wanaotaka kumpeleka Hai kwenda kugombea Ubunge ni hao mafisadi ambao tayari Kilimanjaro wamepandishwa kama wahujumu uchumi. Hicho ndicho kinamfanya Mheshimiwa Lema leo aweweseke…

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Lema nimeshazuia taarifa, nitakupa baadaye.

MHE. GODBLESS J. LEMA: Ajenge hoja, zuia matusi Mwenyekiti.

MWENYEKITI: Sasa unabishana na Kiti Mheshimiwa Lema?

MHE. GODBLESS J. LEMA: Zuia matusi Mwenyekiti.

MWENYEKITI: Dkt. Mollel wewe ni Daktari tunategemea utatoa mchango kwa kutumia lugha ya Kibunge.

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Lema aliwatukana hapa Mawaziri.

MWENYEKITI: Wewe Jacqueline Msongozi kaa kimya. Endelea Mheshimwa Mollel. (Makofi)

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakusheshimu sana lakini tunajua kuna watu wanafadhiliwa kuingia kwenye siasa na watu wachafu na ndiyo tunawadhibiti. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Kama ulivyonunuliwa wewe.

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo la siasa shirikishi ni kama kazi ambayo nchi yetu leo imefanya kuwa na Muswada ambao utafanya leo mwanamke wa Tanzania hii ijulikane ni mfumo gani utamfanya afike hapa Bungeni na siyo aletwe kutoka mfukoni mwa watu wachache. Leo tumepitisha Muswada ambao utafanya rasilimali za vyama vyetu, tuna vyama ambavyo akigombana Mwenyekiti na watu wengine hatujui mwisho wa siku mali ziko wapi. (Makofi)

WABUNGE FULANI: Ooooooooo.

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, hizo ndiyo siasa shirikishi tunazosema. (Makofi)