Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi niweze kuchangia katika Wizara hii ya Katiba na Sheria. Pia ningependa kuchukua fursa hii kuipongeza Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa hotuba nzuri iliyoonesha weledi na uzamifu katika suala zima la Katiba na Sheria. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeeleza yote watu watapiga makofi lakini mwenye macho na masikio atasikia neno hili ambalo watu wa Upinzani tumeeleza Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kusema inahitaji digrii ya ujinga kukubali kupewa kazi bila job description halafu useme huo ni uamuzi wa bosi wako kama anaweza akakupa au asikupe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kuchangia hotuba hii kwa kushauri Serikali mambo yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, tukiwa kama Wabunge kazi yetu kubwa ni kuisimamia na kuishauri Serikali ili iweze kuwatumikia Watanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutekeleza hayo ningependa kushauri na kuwaomba wanasheria waliopo humu na Mawaziri waliopewa dhamna hii waishauri Serikali itekeleze majukumu hayo kwa kumshauri Rais ipasavyo juu ya utekelezaji wa majukumu hayo kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wafahamu wazi kwamba Urais ni taasisi na siyo mtu binafsi.
Mheshimwa Rais tamko lolote atakalolitoa iwe ni kwa masihara au yupo anakunywa chai au anafanya kitu chochote kwetu sisi tunaiona kama ni agizo na tunaichukulia kama ni sheria, kwa hivyo, Mawaziri wahakikishe kwamba Rais wao anapotoa matamko basi yawe ni ya kujenga na siyo kubomoa Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kwamba suala la uendeshwaji wa nchi hii, tukiangalia suala la sukari, suala la vyombo vya habari, suala la utekelezaji wa haki za binadamu, uendeshwaji wa mahakama ni suala ambalo kimsingi Rais wa nchi hii alipaswa kukalishwa chini na kuelezwa ni lipi aliongee kwenye jamii ambalo mwisho wa siku litaleta matunda na siyo kuibomoa nchi hii na kuirudisha mwaka 1980 enzi za uhujumu uchumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, madhara makubwa, leo asubuhi tumepata taarifa kwamba bei ya sukari imefika shilingi 3,200...
MHE. SALOME W. MAKAMBA: Na hii nayo inasababishwa na tamko ambalo Mheshimiwa Rais alilitoa, tunaamini matamko, sheria, kanuni na taratibu za nchi hii zinafanyika kwa kushirikisha wadau, endapo tatizo au suala la sukari na ukuzaji wa viwanda lingeshirikisha wadau ambao ni watumiaji wa sukari pamoja na wafanyabiashara wa sukari, huenda tusingefikia kwenye hatua hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya mahakama zetu tukubaliane mbali na itikadi zetu za kisiasa ni tatizo ambalo linahitaji kuangaliwa kwa umakini wa hali ya juu. Tunakosa uhuru wa mahakama kwa sababu mahakama hizi kinyume na sheria mbalimbali zilizowekwa ikiwa ni pamoja na sheria za kimahakama na uendeshaji wa nchi hii zimekosa uwezo na uwezeshaji. Nimeshangaa sana Mheshimiwa Mbunge aliyepita aliposema kwamba tusiongelee kwa sababu hii ni mihimili inayojitegemea, lakini sisi kama Wabunge ndiyo tunaopitisha bajeti ambayo inakwenda kuiendesha hiyo mihimili mingine. Kwa hiyo, ni jukumu letu kuhakikisha tunatetea na tunasimamia maslahi ili mihimili hii iweze kuwa independent na iweze kufanya kazi kwa ufanisi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mahakama zetu zimekuwa zikikabiliwa na changamoto za miundombinu, malipo ya wafanyakazi na madaraja ya mahakimu; mahakimu wawili wana cheo kimoja, wana daraja moja lakini wanalipwa mishahara tofauti. Suala hili linapaswa kuzungumziwa humu kinyume na mjumbe aliyetoka kuongea anasema kwamba huo ni mhimili unaojitegemea sijui kama yeye ana mfuko wa kuwapelekea mahakama pesa hizo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Idara ya Mahakama inakabiliwa na changamoto kubwa ya rasilimali. Mwaka wa fedha uliopita Wizara ya Katiba na Sheria ilipangiwa fungu lakini pesa hazikupelekwa ndiyo tunaona inazidi kudorora siku hadi siku. Tumeshuhudia kwenye kesi za uchaguzi, Majaji wanakosa impartiality katika decisions zao, ni kwa sababu ya umaskini wa hali ya juu ulioko katika ngazi ya mahakama. Mahakimu wanapewa baiskeli kwa ajili ya kwenda kazini, wanakosa nyumba, hawawezi kujikimu na hii inapelekea kushindwa kusimamia majukumu yao wakiwa kama mhimili wa Serikali unaojitegemea. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijatoka kwenye suala la mahakama mwaka 2012 ulitolewa waraka ambao ulikuwa unaongelea kada ya Mtendaji wa Mahakama. Lengo la kuwa na kada ya Mtendaji wa Mahakama ilikuwa ni kuboresha utendaji kazi wa kiutawala katika ngazi ya Mahakama. Kinyume na mategemeo, kada hii imeshindwa kutekeleza majukumu yake badala yake hali imezidi kuwa mbaya lakini watu hawa wanalipwa na Serikali. Ningeomba Waziri wa Katiba na Sheria aliangalie suala hili kwa umakini sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kabisa naomba niongelee suala la Law School. Tanzania tumekuwa na mfumo ambapo mwanafunzi anapomaliza shahada yake ya sheria analazimishwa kwenda kusoma Law School, lakini Law School imekuwa tofauti na shahada ya sheria. Tanzania vyuo vinavyotoa shahada ya sheria viko Mwanza, Mbeya, Arusha na maeneo mbalimbali na Law School ya Tanzania iko Dar es Salaam. Wanafunzi wanalazimishwa kusafiri kutoka huko wanakosomea ambako walichagua mpaka Dar es Salaam kwa ajili ya Law School. Usipofanya hivyo, pamoja na miaka minne aliyoipoteza wakati unasoma shahada yako ya sheria mwanafunzi yule hawezi kutambulika kama ni mwanasheria kamili na hawezi kupata ajira. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mbali na tatizo hilo, wanafunzi hao walio wengi walikuwa wanasomeshwa kwa kutumia mkopo. Cha kusikitisha ni kwamba anapokwenda Law School suala la mkopo inabidi lifanyiwe pre-assessment tena na wanafunzi hawa hawapewi mkopo. Kwa taarifa tu, sasa hivi ada ya Law School ni shilingi milioni moja laki tano na zaidi. Watoto waliokuwa wanasoma shahada ya sheria walikuwa wanalipiwa mkopo na Serikali lakini linapofikia suala la kwenda Law School linakuwa ni jukumu la mzazi kujua yule mtoto atafikiaje kwenye hatua hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili inabidi liangaliwe kwa umakini. Tunayo majengo yako UDOM pale wanakaa buibui, tunayo majengo na watu ambao wanaweza kutekeleza suala hili, lakini leo watu wachache wamejirasimisha zoezi hili wameweka Law School Dar es Salaam. Watu wanalazimishwa kusafiri mpaka Dar es Salaam, hawana makazi, wengine hawajawahi hata siku moja kufika Dar es Salaam, wanalazimishwa wakakae pale wasome Law School kwa sababu kuna maprofesa wachache au watu wachache wanaotaka kunufaika na mfumo huu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda suala la Law School lishirikishe wadau hasa wanafunzi wanaokwenda kwenye shule hiyo. Pia ifahamike kuna watu ambao hawakusoma Law School zamani lakini leo kila gazeti utakalolishika linatangaza kazi lazima uwe umepitia Law School. Kwa yule ndugu yangu ambaye hafahamu kiingereza kama alivyoomba afundishwe Law School ni ile shule ya sheria ambayo ni lazima uende kusoma ili uweze kuwa Wakili kwa mujibu wa Law School Act ya mwaka 2007.
MHE. SALOME. W. MAKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, namuone huruma sana Mheshimiwa anayesimama na kusema kwamba anakaa Dar es Salaam lakini hajawahi kuona mahakama. Mahakama si kama tangazo la Vodacom au la Tigo linalobandikwa kwenye jukwaa.
MHE. SALOME. W. MAKAMBA: Mahakama ni institution ambayo iko kwa mujibu wa sheria na anachoelezwa ni fact kwa mujibu wa sheria. Unaweza ukakaa Dar es Salaam ukafahamu ratiba ya vigodoro Dar es Salaam nzima lakini usijue ziko mahakama ngapi.
MHE. SALOME. W. MAKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.