Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii, nami niweze kuunga mkono azimio hili la kupandisha haya mapori na kuwa hifadhi. Kilichonisukuma niweze kuunga mkono maazimio haya, sisi Mkoa wa Kigoma tumeathiriwa sana na hili pori lililokuwa la Biharamulo. Hili pori la Biharamulo lilikuwa linatufanya mabasi yanapopita pale ya abiria lazima uende na Askari wakiwa wanalinda. Ukiwa na gari lako la binafsi, uende na Askari wakulinde mpaka utakapofika maeneo ya Kibondo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa kulipandisha hadhi hili kuwa hifadhi, tuna uhakika kwamba mambo yataanza kuwa mazuri kwa sababu majambazi kutoka Burundi na Rwanda wamekuwa wakijificha mle. Kwa hiyo, ndiyo sababu iliyonifanya nivutike kuunga mkono hoja hii.

Mheshimiwa Spika, siyo hivyo tu, hata haya mapori mengine tunazo faida nyingi za kiuchumi kwa sababu nazo zitakuwa ni sehemu ya utalii, lakini tour guide wetu watapata ajira na mahoteli yataweza kuwekwa pale kwenye baadhi ya maeneo na vile vile mapato utalii nayo yataongezeka. Faida nyingine, tutaendelea kutunza mazingira kwa sababu, kwa kuwa ni mapori watu wamekuwa wakienda kufanya shughuli mbalimbali za ufugaji, wanalima, wanakata miti, wanakata mkaa ndani ya yale mapori. Kwa hiyo, hifadhi nzima inakuwa imeharibika. Kwa hiyo, sababu hizo zinasababisha tuweze kuunga mkono azimio hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kikubwa zaidi ni faida za kiuchumi tutakazozipata kwenye mapori haya. Mengine nashukuru kwamba kwa kuwa yanaenda TANAPA na tuna Mkurugenzi pale Kijazi yuko imara kuweza kuyasimamia, kwa hiyo, naye tunampa wito kwamba aweze kuyawekeza miundombinu ndani ya hifadhi ili nayo hadhi yake iweze kuwepo. Zaidi elimu iweze kutolewa kwa vijiji vinavyozunguka kwa sababu wengine walikuwa wanakidhi mahitaji yao mle. Kwa hiyo, elimu iweze kutolewa kwa vile vjiji vinayozunguka ili faida ya hifadhi hizi ziweze kuonekana.

Mheshimiwa Spika, sitaki kupoteza muda, naunga mkono maazimio haya. (Makofi)