Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii ambayo umenipatia. Naomba niwashukuru wote ambao wamepata nafasi ya kuchangia, lakini pia niwashukuru kwa sababu asilimia kubwa ya wachangiaji wameunga mkono hoja na sisi ambao tumeleta hoja hii tumefarijika kuona kumbe ulikuwa ni mtazamo wa kila mtu kuona umuhimu wa hifadhi hii kuwa National Park.

Mheshimiwa Spika, kama alivyomalizia kusema Mheshimiwa Angelina Mabula, watu wengi ambao hawajawahi kufika BBK hawaifahamu vizuri. Ukiwa BBK upande ambao tunapakana na nchi jirani kuna vijiji vinakwenda mpaka kwenye mto, mpaka wetu ni mto, lakini ukivuka mto peke yake unaingia kwenye BBK hizi ambazo tunazungumzia hii Kimisi, Burigi pamoja na Biharamulo. Maana yake ni kwamba, upande wa pili palikuwa na watu ambao wana access ya moja kwa moja na game reserve, lakini upande wetu huu kwa sababu, mpaka ni mrefu na kwa sababu ya uwezo ambao TAWA walikuwa nao tulikuwa tunshindwa kwa kweli kimsingi kusimamia ulinzi vizuri.

Mheshimiwa Spika, sasa tunafarijika kuona kwamba, baada ya kuwapatia TANAPA na kama walivyosema Wajumbe wengi ni kwamba, TANAPA kimsingi wanazo financial muscles ambazo zitatusaidia sana kwenye kuimarisha ulinzi. Katika kuhakikisha kwamba, hili linaungwa mkono na kauli hii, baada tu ya sisi kuonesha kwamba, tunataka kuichukua hii kuwa TANAPA, tayari TANAPA wamekwishatengeneza kilometa 121 za barabara, wamekwishapeleka magari matano kwa ajili ya kuimarisha doria, wamenunua maboti mawili kwa ajili ya usimamizi kwenye Ziwa Burigi na Ziwa Ngoma. Pia lakini tayari wametambua maeneo nyeti ya uwekezaji kwa ajili ya ujenzi wa hoteli na wameongeza idadi ya wafanyakazi katika eneo hili na kupeleka wafanyakazi 70. Kwa hiyo, utaona utayari wa TANAPA katika kuhudumia eneo hili ni mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la ushirikishwaji; tangu tulipokuja na wazo hili tumezitumia Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya, lakini Viongozi wa Vijiji wa maeneo husika. Wote hawa wametumika katika kutoa elimu na kuwaeleza faida ambazo zitapatikana kutokana na eneo hili kuwa hifadhi ya Taifa. Hata hivyo, elimu itaendelea kutolewa kwa sababu, elimu ni suala la kudumu. Naamini kwamba, wananchi wa maeneo haya wamejiandaa vizuri zaidi kupokea eneo hili kuchukuliwa na TANAPA kwa sababu za historia ya TANAPA yenyewe namna inavyofanya kazi, lakini faida ambayo wanaipata.

Mheshimiwa Spika, tunategemea watapata faida gani; la kwanza, tunaamini kwamba, eneo lile likishafanyika uwekezaji wa kutosha, ukiacha suala la usalama lipo suala la biashara. Maeneo yale yatachangamka sana kibiashara, kutajengwa hoteli za ndani na nje ya eneo hilo ambazo zitafanya mzunguko wa pesa katika eneo hilo kuwa mkubwa, lakini tutaimarisha zaidi cultural tourism. Maeneo mengi sana ukiwa unatoea Arusha ukija kufika Serengeti wananchi wa maeneo yale wanaona umuhimu wa uwepo wa Ngorongoro na Serengeti kwa sababu, wakati watalii wanaelekea kwenye kutalii Serengeti na Ngorongoro wanapita kwenye maeneo ya wananchi na kuona namna ambavyo wananchi wanashiriki kwenye utalii. Vile vile, tunaamini kwamba, usimamizi mzuri wa mazingira utaimarika ikiwa ni pamoja na ongezeko kubwa la ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Msigwa ameonesha dalili ya kwamba, nikitafsiri vizuri lugha yake ni kama anaona kunafanyika upendeleo kupeleka TANAPA sasa hivi BBK na kuacha REGROW, Mheshimiwa Waziri wangu atazungumzia vizuri kuhusu REGROW, Lakini nataka nimtoe wasiwasi kwamba, nchi hii ni moja, mtazamo ambao Serikali inao kuhusu Kusini ni mtazamo uleule ambao inao kuhusu Kaskazini,
kuhusu Magharibi na sehemu nyingine zote na kwamba, haya hayafanyiki ili kuondoa umuhimu wa eneo la Southern Circuit.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)