Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa dakika hizi chache nilizozipata. Kwanza naomba kuunga mkono hoja hizi za Kamati zote mbili lakini nitaongea haraka haraka sana kwa sababu ya muda.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza, Kamati ya Nishati na Madini imezungumza mambo mengi sana ya msingi na miongoni mwa mambo ambayo nimeyapenda sana ni suala zima la kudhibiti utoroshwaji wa madini ambapo imeweza kuipongeza Serikali. Nami pia nichukue fursa hii kuipongeza Serikali kwa kitendo cha kujenga ule ukuta wa Mererani ambapo tanzanite ilikuwa inatoroshwa kwa kiasi kikubwa sana. Wakati wa Kamati Maalum tuliweza kupewa taarifa kwamba miji mingi ya Kenya ukiwemo Mji wa Naivasha umeendelea kwa kiasi kikubwa kwa sababu ya madini ya tanzanite yanayotoroshwa kutoka Mererani Tanzania, leo ni mji bora kabisa kule Kenya. Kwa hiyo, naipongeza Serikali kwa kitendo hiki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi hizo bado kuna uhafifu katika kudhibiti madini mengine yakiwemo madini ya blue sapphire ambayo yanapatikana kule Tunduru, Mkoani Ruvuma. Kule Tunduru kuna watu wa Sri Lanka wengi sana ambao wananunua madini haya na wanayapeleka kwao wanayaunganisha wanasema haya madini yanatoka Sri Lanka, blue sapphire inatoka Tunduru. Niitake Serikali kama kweli tunahitaji kudhibiti sekta hii ya madini ambayo imenufaisha nchi nyingi duniani basi tudhibiti madini ya blue sapphire kule Tunduru yasiweze kutoroshwa hovyo hovyo na kupelekwa Sri Lanka na zaidi kuweka label ya Sri Lanka kwamba yanatokea pale Sri Lanka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine nizungumzie suala la miradi hii ya gesi. Nisikitike kwamba Kamati imesema ni sekta ndogo ya gesi na sekta ndogo ya madini. Nashangaa, kwa nini iitwe sekta ndogo? Kwa sababu kama kweli tunahitaji kuitumia gesi sawasawa, nchi za wenzetu kwa mfano, Qatar na nchi zingine zimeweza kuendelea kwa kutumia uchumi wa gesi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naiomba Serikali tuwekeze katika miradi ya gesi ambayo ilianza kuwekezwa miaka sita, saba iliyopita. Kule Mtwara na Lindi kuna ule mradi wa LNG, nashangaa kwamba Serikali iko kimya sana, haiendelezi mradi ule. Ule mradi ulikuja kuleta ajira nyingi sana kwa wananchi wa Mikoa ile ya Kusini, wananchi wa Mkoa wa Lindi. (Makofi)

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Maftaha kuna taarifa, Mheshimiwa Heche.

T A A R I F A

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, sina uhakika sana na maelezo yake na kwa kawaida huwa nazungumza mambo ambayo nina uhakika nayo.

MHE. RICHARD M. NDASSA: Taarifa.

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba unilindie muda wangu.

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, taarifa inabidi akishachangia mtu akishapewa taarifa aipokee kwanza ile taarifa aanze kuzungumza ndiyo anapewa taarifa nyingine. Mheshimiwa Ndassa.

T A A R I F A

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee kwa sababu muda wangu ni mchache sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilichokuwa nazungumza hapa ni kwamba sekta ya gesi na mafuta ni muhimu sana, haziwezi kuitwa ni sekta ndogo. Naamini kama kweli kwa sababu taarifa ya Kamati imezungumza hapa kwamba Serikali ina mpango wa kuongeza megawatts za umeme na mipango ya Serikali inasema ikifika 2020 basi tuweze kuwa na MW 5,000 lakini taarifa ya Kamati inasema mpaka 2020 tutakuwa na megawatts zisizozidi 2,780. Kwa hiyo, naishauri Serikali kwa sababu tuna sekta ya gesi Mikoa ya Kusini, mpango ule wa kujenga zile plant za Lindi, kuendeleza zile plant za Mtwara, tujenge plant ya umeme Kanda ya Kusini ili tuweze kuziongeza hizi megawatts Taifa hili liweze kuondokana na tatizo hili la umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mipango ya Serikali ya kujenga Stigler’s Gorge, ni mipango mizuri kwa sababu lazima kama Taifa kuwe na miradi ya kielelezo lakini bado ikifika 2020 hatutakuwa na megawatts zile ambazo tunazihitaji. Kwa hiyo, kwa kuwa miradi ya gesi iko tayari maeneo ya Kusini, Serikali ijenga plant za umeme kwa kutumia hii gesi yetu ambayo Mwenyezi Mungu ametubariki. Bahati njema kwamba Mikoa ya Kusini hivi sasa tayari Serikali imeshaiunganisha katika gridi ya Taifa. Tukijenga plant Mtwara na Lindi tutaweza kusafirisha umeme mwingi tukaingiza katika gridi yetu ya Taifa na tukaondokana na tatizo hili la kukosa umeme wa uhakika.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine naomba nizungumzie…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)