Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, cha kwanza, naomba niwape pole wananchi wangu wa Ulanga kwa hii hali ya mvua inayoendelea, barabara hazipitiki, mafuriko kila kona. Pia naomba niwapongeze wafanyakazi wa Halmashauri kwa kukubali kufanya kazi katika mazingira magumu kiasi hicho. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mwakyembe kaka yangu, Wilayani kwangu hakuna jengo la Mahakama ya Wilaya, wanatumia jengo la Mkuu wa Wilaya, naomba unijengee. Hakuna nyumba za watumishi wa mahakama, wananchi wangu wanatembea umbali mrefu kufuata hizi huduma za mahakama. Kwa hiyo, naomba nisaidie hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mara ya mwisho wakati nachangia tarehe 25 ilitokea tafrani ya kutoeleweka kwa lugha ambayo niliitumia, nilisema Mheshimiwa Pinda ametokea dirishani. Waheshimiwa Wabunge mtakubaliana na mimi kuwa kiswahili kilianzia maeneo ya Pwani kwa hiyo sisi kwetu Upogoroni maneno ya kiswahili yalichelewa kufika, matokeo yake tuna umaskini kidogo wa maneno.
Mheshimiwa Naibu Spika, nia yangu ilikuwa kusema hivi, sisi Chama cha Mapinduzi hatuna msalie Mtume katika maslahi ya wananchi. Inapotokea sintofahamu mahali tunakuita tunakuhoji, ukituridhisha tunakuruhusu uendelee. Kwa hiyo, wapinzani naomba mtuige na ndiyo maana tunaendelea kutawala nchi hii kwa sababu ya mfumo huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna msemo usemao mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Naomba nimpe hongera baba mkwe wangu Mheshimiwa Mbowe kwa kuwaruhusu wapinzani kuendelea kuchangia Bungeni kutokana na ushauri niliompa. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna Mbunge atakayepinga ni mimi niliyeleta semina humu Bungeni ya Mwenyekiti kasema ndiyo iliyopelekea Wabunge wa Upinzani kuruhusiwa kuchangia. Nilisema kuwa nina umbo dogo lakini nina mambo makubwa. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Lissu pamoja na kujinadi amebobea sheria alishindwa kumshauri Mbowe ili waendelee kuchangia. Mheshimiwa Mchungaji Msigwa pamoja na uchungaji wake alishindwa kumshawishi Mheshimiwa Mbowe waendelee kuchangia humu Bungeni. Mheshimiwa Sugu pamoja na kuzaliwa mjini kashindwa kumshawishi Mheshimiwa Mbowe kuendelea kuchangia humu Bungeni, ni Mlinga pekee ndiye aliyemshawishi Mheshimiwa Mbowe mpaka Kambi Rasmi ya Upinzani wakaendelea kuchangia humu Bungeni. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, hii inakuwa funzo kwa Wabunge wa Upinzani, bila ya mimi mngekuwa mabubu mpaka Bunge hili linaisha. Naomba mpelekeeni salamu baba mkwe wangu, najua haingii Bungeni ananiogopa, aingie mimi ni mtoto wa mjini, nimeshasahau. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge wote ni mashahidi, hakuna Mbunge aliyekuwa anaikashifu Zanzibar kama Mheshimiwa Tundu Lissu. Wanasema hivi, ukitaka umuumize adui zaidi jifanye kuwa rafiki yako. Mheshimiwa Tundu Lissu alitumia njia ile akaona hailipi, akawageuza Wazanzibar kuwa rafiki yao matokeo yake akawashawishi wasiingie kwenye uchaguzi, CUF kwisha Zanzibar. (Makofi)
Kwa mara ya kwanza wakati ninamsikia Mheshimiwa Tundu Lissu kuwa ni mwanasheria nilishtuka lakini nilipoingia Bungeni nilisikitika baada ya kuhakikisha kweli ni Mwanasheria na Wakili. Hofu yangu, kama ni Mwanasheria na Wakili ambao tunawategemea kutetea na kututunzia sheria mcharuko kiasi hiki hao waalifu wakoje?
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, wote ni mashahidi wa ukanyagaji wa demokrasia unaofanywa na chama ambacho Tundu Lissu ndiyo anakitetea kwenye upande wa sheria. Tumeshuhudia Mheshimiwa Lowassa alivyoingia CHADEMA, ameingia siku hiyo hiyo, amepewa fomu ya Urais siku hiyo hiyo, ametangazwa siku hiyo hiyo. (Makofi)
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, wanachama wa CHADEMA Jimboni kwangu walikuwa wanasema mimi nimerithishwa, nikawauliza kati ya mimi na Lowassa ni nani aliyepata fursa ya kugombea kwa kufuata taratibu za demokrasia? Nimepita kura za maoni, sawa, tulikuwa wagombea nane nikawapiga, nikaenda Uchaguzi Mkuu nikakutana na mgombea wa CHADEMA ana umri wa miaka 40 hana jino hata moja nikampiga.
KUHUSU UTARATIBU....
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Jamani nilishasema Upogoroni maneno yamechelewa kufika, sijajua kuwa hilo neno lilikuwa zito kiasi hicho, nimelifuta. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nashangazwa na Kambi ya Upinzani kuhoji habari ya Escrow mpaka leo hii wakati baba mkwe wangu alichukua gari ya Serikali, mafuta ya Serikali, alienda kuchukua dola milioni moja Kenya, Nairobi, mbona Kambi ya Upinzani hamlizungumzii hilo?