Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kujadili Hotuba za Kamati ya Nishati na Madini, pamoja na Ulinzi na Mambo ya Nje. Kwangu nijikite tu kidogo kwa sababu ya muda niongelee tu kidogo kuhusu suala la Stiegler’s gorge. Tunapokuwa tunaongelea long term investment haiwezi kuwa ni kitu ambacho kinaweza kuzuka tu katika kipindi kifupi, tunayo short term plan, tunayo medium na zile long term. Wakati tunajadili suala la long term plan wakati huo short term plan zile zinaendelea. Kwa hiyo, unaponiambia kwamba huu mradi utakamilika baada ya miaka saba ni kipindi kifupi sana hasa kwa sisi ambao tunaona kuna faida kwa uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni vizuri pia watu ambao wanatoa hoja hizi wakawa wanasubiri na kusikiliza wenzao wanaweza kuzipangua vipi zile hoja zenyewe. Kwa sababu unazungumzia suala la MW 300, hata hivyo, sasa hivi Taifa halipo kwenye crisis, Taifa tayari linao umeme wa kutosha na pengine ni wa ziada. Kwa hiyo tunapoongelea mipango mikubwa, ni lazima tuongelee mipango mikubwa ya miaka mingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapoongelea gesi lazima useme hii gesi ya MW 300 life span yake ni ya muda gani? Inaweza ikawa kumbe ina life span ya miaka 20, lakini unapoongelea Stiegler’s gorge vile vile na yenyewe uende uone kwamba ina life span ya miaka mingapi? Kwa hiyo huwezi ukavilinganisha vitu ambavyo unaweza ukavifanya kwa short term plan, medium plan na long term plan. Kwa hiyo, wakati mwingine tunapokuwa tunaizungumzia hii miradi na hasa miradi mikubwa, kwa sababu tayari Taifa limeshajipambanua, tunaenda kwenye viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda ni lazima tupate nishati ya kutosha, kwa hiyo hata ingekuwa huu mradi unaanza baada ya miaka 15 tunachokiangalia ni viability ya business yenyewe na tunachoangalia ni sustainability ya business yenyewe. Kwa hiyo, mwisho wa hapo ndio unaweza ukazijenga hoja zako vizuri. Sisi hatuna crisis kusema kwamba kesho ni lazima tufanye ili niweze kuja ku-support kwenye viwanda ambavyo tunataka kuviendeleza. Kwa hiyo, kuna tabia ya kuwa sisi Wabunge tunajenga hoja unapotaka kujibiwa wewe unakuwa haupo, matokeo yake sasa next time unakuja unalijadili tena suala lile lile kitu ambacho si sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine niende kwenye madini. Tunalo suala la Liganga na Mchuchuma. Kwa kweli nimeona Wabunge wengi walikuwa wameizungumzia, lakini kuna haja Serikali ikaweka concentration kubwa na kama kwenye mpango wa maendeleo ilivyokuwa imezungumzwa kwamba kuna haja ya kujenga kiwanda cha kufua chuma pale Liganga. Ningeomba Serikali ijikite kwa sababu hadithi hii imekuwa ni hadithi ya muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nina imani Serikali ya Awamu ya Tano itaweka concentration kubwa na nina imani kwamba ni Serikali sikivu hiki Kiwanda cha kufua Chuma pale, kitakuja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niingie kwenye suala la REA, REA wanafanya kazi nzuri, japo upo upungufu wa hapa na pale lakini kazi inayofanywa ni nzuri na ni kubwa. Sisi wote tunatoka kwenye majimbo, tunaona jitihada zinazofanyika za kuhakikisha kwamba vijiji vyetu vingi vinapata umeme na vita-stimulate uchumi wa maeneo ambayo sisi tunafika. Kwa hiyo tuipongeze Serikali kwa kazi nzuri inayoifanya na tujaribu kuitia moyo na kuwatia nguvu ili waweze kuzidisha mapambano na hatimaye tukaondoa ule umaskini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye suala la ulinzi. Kule maeneo ya Ziwa Nyasa hakuna doria yoyote ambayo inafanyika, hatuna boti la kiulinzi. Niiombe Serikali itupatie ulinzi kwenye maeneo yale na maeneo ya maziwa mengine ili kuweza kuondoa sintofahamu ambazo zinatokea hivi sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga hoja mkono. (Makofi)