Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Ajali Rashid Akibar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. AJALI R. AKBAR: Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi naona dhamira ya Serikali ya REA III kwa kweli ni nzuri, isipokuwa kuna challenge ndogondogo ambazo sisi kama Wanakamati baada ya kutembelea tumekutana nazo. Kwa mfano ukosefu wa nguzo, nyaya, mashine umba; haya ndiyo matatizo ambayo yamejitokeza kwa wingi sana wakati tulipotembelea miradi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama hii haitoshi kuna kurukwa kwa vijiji kama ambavyo Wajumbe wengi wamezungumza. Kwamba vijiji vingi vimerukwa kutokana na kukosekana kwa scope of work. Kwa hiyo, niiombe tu kwamba Wizara ifanye jitahada ya kuhakikisha kwamba sasa hili tatizo la kurukwa vijiji kutokana na kukosekana kwa scope of work lisirudiwe tena, maana yake liende hatua kwa hatua, kama Mheshimiwa Waziri anavyokuwa akizungumza siku zote.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kuhusu hawa Mawaziri wetu; Mawaziri wote kwa kweli wamekuwa wakifanya kazi. Mawaziri wa Nishati wamekuwa wakijitahidi sana kufanya kazi kwa kiasi kikubwa sana, Mawaziri wa Madini wamekuwa wakifanya kwa kiasi kikubwa sana; kwa kweli production inaonekana sasa hivi. Kwa mfano, leo unaweza ukachukulia hoja ya TANESCO. TANESCO leo wana uwezo, wao wenyewe wanajikimu wao, wenyewe wana uwezo wa kulipia bili zao za umeme. Hii ni jitihada kubwa kwa sababu TANESCO haikuwa kufikia hivyo. Ina maana kwamba kuna watu ambao wanafanya kazi ndiyo maana mpaka leo TANESCO inafanya kazi kiasi hicho na ina maana hawa vijana wanajitahidi kwa kiasi kikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kwenye makusanyo, maduhuli yamekuwa yakionekana kwa kiasi kikubwa sana kwa upande wa madini, ina maana kwamba watu wa Madini, wamekuwa wakifanya kazi kwa kiasi kikubwa na ndio maana maduhuli, yamekuwa yakionekana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo tulikuwa tunazungumzia, ni kuhusu Jeshi letu. Hili Jeshi letu lilikuwa la wapigania uhuru wakati ule wa enzi za Mwalimu Nyerere. Siku moja niliwahi kuongelea kwamba tuangalie namna gani sasa hivi hili jeshi letu linaweza likageuka likawa jeshi la kiuchumi, lisiwe jeshi tu ambalo sasa hivi linakwenda kwenye korosho huko Mtwara, badala yake tulitumie Jeshi hilo Kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, wamchukulie Mheshimiwa Keissy alivyozungumza, kwamba tulitumie lile jeshi kiuchumi, ina maana kwamba watu wote ambao tumewaondoa kwenye mikono ya mabeberu sasa hivi ni wakati wao wa kurejesha zile fadhila ambazo tulikuwa tumewaondoa katika mikono hiyo maana hakuna hata mtu mmoja anayekuja kutushukuru. Sasa kama tuna nguvu kazi ya kutosha, tuna vijana wa kutosha, kwa nini na sisi tusiwe kama wanavyofanya mabeberu wengine wa Ulaya? Kwa hiyo tuangalie, namna gani hawa vijana wetu ambao wana nguvu za kutosha tunaweza tukawabadilisha likawa ni jeshi la kiuchumi ili sisi tuishi maisha mazuri kama wanavyoweza kuishi wengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo nimeliona ni kuwapongeza, pamoja na ukwasi ni kwamba hii, Stiegler’s Gorge hii, kwa kweli umeme tunauhitaji. Nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kuwapa vijana kazi hii na hawa vijana waendelee kuchapa kazi, haiwezekani moja kwa moja wewe ukawa unafanya kazi usisikie kelele, haiwezekani; maana mti unapopolewa ndio ambao una matunda huo. Kwa hiyo wakiona kwamba wanapigwa mawe basi wajue kwamba chochote wanachokifanya, waweke jitihada ili kuhakikisha kwamba hili bwawa la Stiegler’s Gorge linafanya kazi na linazalisha vizuri zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kuhusu ule mradi ambao tulikuwa tumekubaliana katika Kamati, kwamba zile megawatt 400, Serikali ifanye jitihada na yule Mkandarasi aanze kazi ili kuhakikisha kwamba zile megawatt 400 pale Mtwara zinajengwa kwa haraka sana; ili kuhakikisha kwamba umeme unapatikana kwa wakati kama vile ambavyo tumekubaliana na kama vile ambavyo wananchi wengi wana uhitaji umeme.

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Kengele imeshagongwa Mheshimiwa, ahsante sana.

MHE. AJALI R. AKBAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga mkono hoja.