Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI MHE. HALIMA JAMES MDEE (MB)

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

TAARIFA YA KAMATI YA HAKI, MAADILI NA MADARAKA YA BUNGE KUHUSU SHAURI LA KUDHARAU NA KUDHALILISHA BUNGE LINALOMKABILI MHE. HALIMA JAMES MDEE (MB)

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naanza kwa kusema kuwa naunga mkono Azimio la Kamati.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Halima amekuwa mzoefu mara kwa mara na nianze kusema kwamba Kamati imemuonea huruma kwa kumpatia vipindi viwili. Kama Mwenyekiti alivyoongea ilikuwa iwe zaidi ya hapo ila tumeona kwa sababu tunakaribia mwisho wa Bunge ndiyo akapewa vipindi viwili kwa kulidhalilisha Bunge kwa kusema kuwa ni dhaifu na yeye akiwa ni mmojawapo wa Wabunge. Kwa kweli halileti maana nzuri sana kwani angeweza kutumia njia yoyote ile kulishauri Bunge bila kusema kwenye vyombo vya habari.

Mheshimiwa Naibu spika, mimi naunga mkono na nasema kuwa Kamati kwa kweli imemhurumia la sivyo ukishapata adhabu kubwa hupaswi kupata adhabu ndogo, inabidi upate kubwa zaidi. Naunga mkono kwa vipindi viwili, ahsante. (Makofi)