Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Naibu Spika,nashukuru kwa kupata nafasi hii ya kuchangia hotuba hii ya Waziri Mkuu. Nimepitia vizuri kitabu hiki cha Waziri Mkuu hasa katika ukurasa wa tisa ambapo amezungumzia mafanikio ya miradi ambayo imefnywa na Serikali hii ya Awamu ya Tano. Moja ya mafanikio aliyoyazungumza ni kuhusu ujenzi wa Standard Gaugeunaoendelea hivi sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatupingani kabisa na mradi huu, tunachokizungumza ni kuhusuproper planning za mradi huu. Ili nchi yoyote iendelee lazima iwe na mikakati endelevu, nchi za uarabuni ambazo zina mafuta, ukiwauliza hata kesho yao baada ya mafuta kwisha, wanafahamu. Kwa sababu wanaingia gharama ku-implement teknolojia ambazo zinabaki kwa wazawa.

Mheshimiwa Naibu Spika,leotunafanya Standard Gauge, asilimia 20 ya labour skills ni Watanzania, asilimia 80 ni Waturuki. Tunasema kwamba mradi huu unatoa ajira kwa Watanzania kwa kiwango kikubwa, labda watuambie Watanzania wataishia kufanya zile kazi ndogondogo za mamantilie na zinginezo, asilimia 80 ya teknolojia kubwa zinafanywa na Waturuki. Kwa hiyo, tunachosema sisi, tuwe na miradi ambayo ina proper planning, tuandae watu wetu kwanza kuingia katika hiyo teknolojia, tupate watu professionals ambao sasa kwa asilimia 90 watakuwa…

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA):Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Devotha Minja kuna taarifa.

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpe taarifadada yangu Mheshimiwa Devotha Minja kwamba, akizungumzia mambo ya ajira wakati wa ujenzi wa SGR, ni very short term yaani kama kuzungumza leo na wakati ule mradi ni wa miaka nenda rudi. Kwa hiyo, azungumzie labda impact ambayo nchi itapata kupitia mradi huu, badala ya kuzungumzia vitu vya leo wakati ule ni mradi wa muda mrefu.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Devotha Minja unaipokea taarifa hiyo?

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani ana muda baadaye anaweza akajibu kama Naibu Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachokisema, tulitegemea, neema ambayo aliisema Rais, kwamba ajira zitabaki kwaWatanzania, asilimia zaidi ya 90 kazi hizi zifanywe na Watanzania, lakini sasa zinafanywa asilimia 20 ambao ni Watanzania. Hoja yangu ni kwamba, tulitakiwa tujiandae kabla ya kuingia kwenye mradi huu, kwa maana kuwaandaa watu ambao wana uwezo wa kufanya hizi kazi kwa ufanisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni suala la mataruma, mataruma hivi sasa ya reli yanatoka China. Hivi tulikuwa na sababu gani ya kukimbiliakuanza mradi huu, badala ya kufufua miradi ya Mchuchuma na Liganga, tukapata mataruma, yakatusaidia, tukaweza kupunguza gharama ya fedha nyingi ambayo sasa hivi inakwenda China badala ya kubaki hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapozungumza miradi hii, inaleta maswali kwa wananchi. SGR, unazungumzia bilioni 16, kwa wananchi wa kawaida tu, ukiwauliza kipaumbele ni nini sasa hivi watakwambia tunataka huduma za afya, ni suala la kisera kwamba, kila kata iwe na kituo cha afya. Katika vituo vya afyakata 4,420, kuna vituo vya afya 513 na katika hivyo 513, vituo 115 ni vya private.

Kwa hiyo, kwa mwananchi wa kawaida ukimwambia unapeleka bilioni 16 kwenye SGR, ambapo hana huduma yoyote ya afya, wananchi wa kawaida hawatuelewi.

Mheshimiwa Naibu Spika,tunasema yote ni mipango, lakini lazima tuangalie basic needs kwa wananchi. Kuna maeneo hivi sasa yanapata maji kwa asilimia tatu, lakini ukimwambia mtu habari za SGR hakuelewi, anataka maji, anataka huduma zaafya. Kwa hiyo, tunasema niproper planning Tanzania kuangalia priorities za nchi na kwa wananchi wake.

Mheshimiwa Naibu Spika,Mheshimiwa Waziri Mkuu amesema kuhusu mradi wa kufua umeme wa Stiegler’sambao utagharimu takriban trioni 6.5. Tulikuwa na mradi wa Kidunda, ambao ulikuwa una uwezo wa kuzalishamegawatts 20 za umeme, ulikuwa na uwezo wa kuzalisha maji yatakayotumika kwa wakazi wa Dar es Salaam kwa ajili ya viwanda, kwa ajili ya mashamba ya umwagiliaji, lakini hivi sasa tumeacha huku, tunakimbilia kwenye Stiegler’s. Kwa hiyo, ni wakati ambao tunataka kusema ni kwanini Serikali inakuwa na miradi mingi halafu implementation yake, mingine inaachwa, mingine inapewa kipaumbele!

Mheshimiwa Naibu Spika,kama suala ni umeme, tungeanza na Kidunda, watu walishalipwa fidia, ndipo twende kwenye Stiegler’s, tuangalie kwamba tuna upungufu wa umeme kiasi gani, ndipo tungeanza mradi huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mambo ambayo tukijiuliza, umeme wa maji siyo reliable siku hizi, kwa nchi nyingi sasa hivi kutokana na mabadiliko ya tabianchi. Tungeweza tukafikiria zaidi hata kuwa na umeme, sisi tuko chini ya equator, kuwa na umeme wa jua, umeme wa upepo na kadhalika, badala ya hivi sasa nguvu zote, Kidunda wananchi wamelipwa, wameachwa kama walivyo, sasa hivi nguvu za Serikali zinaenda kwenye Stiegler’s.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikiliza Waziri Mkuu pia amesema suala la ununuzi wa ndege. Ndege nneBombardierzimegharimu zaidi ya bilioni 280, lakini hivi karibuni tumeambiwa, maintenance ya ndege hizi zimetumika zaidi ya bilioni 14, hivi tunatengeneza faida? Hivi ni biashara kwenye ndege! Airbus moja ambayo ni takribani bilioni 200 iliyokuja juzi, tunajiuliza iko wapi! Tuliambiwa italeta watalii kutoka Marekani, kutoka Uingereza kutoka wapi, hivikwa nini hatuioni ikifanya shughuli hizo, kwa nini hatuioni sasa hivi ikifanya shughuli hizo?

Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Waziri atakapokuja kujibu atueleze iko wapi hiyo ndege. Kwa sababu ukisoma kwenye mitandao unaambiwa mara imeuzwa Kenya, mara iko kwenye matengenezo, mara iko garage, mara inapakwa rangi. Ndege iliyokuja juzi, shughuli zote za nchi zikasimama kwa sababu ya ndege moja, ambayo imekuja nchini. Leo hatuelewi kwamba huo uzalishaji wa ndege hii mpaka sasa umeingiza faida kiasi gani.

Mheshimiwa Naibu Spika, zipo taarifakwenye mitandao, mara inaonekana inabeba nyama kutoka Mwanza, tunataka tuambiwe, kwa sababu zimenunuliwa na kodi za Watanzania, ziko wapi ndege hizi za kuleta watalii ziinue utalii wa nchi hii, inafanyakazi gani hivi sasa?Ndiyo ugomvi wetu, tunahitaji fedha za Serikali zitumike vizuri, badala ya kuleta ndege miezi mitatu toka Januari, ime- ground, badala ya kwenda huko nje, ikafanya yale ambayo Serikali imesema, matokeo yake tunayasikia tu ya mitandao yanayoendelea. Kwa hiyo, watu wanataka kufahamu specificni kitu gani kinaendelea.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Devotha Minja, unapokea taarifa hiyo.

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Naibu Spika, ana muda wa kutosha kuja kujibu. Nilitegemea angeniambia airbus iko wapi sasa hivi ambayo Watanzania wanataka kujua. Sheria za kimataifa zinasema ili uende nchi kama Amsterdam na kwingineko kwenye mataifa yaliyoendelea lazima uwe na ndege tatu, kwa maana ya mbili ziwe angani na moja iwe reserved. Sasa ya kwetu tutaiweka reserved tukisubiri zingine zije ndipo zianze kuruka, tunasema ni kuilaza pesa chini. Nafikiri atakuwa na muda mzuri wa kunieleza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukienda kwenye hali ya kisiasa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

T A A R I F A

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka, kengele ya pili imeshagonga nilikuwa nampa dakika yake moja ili aweze kumalizia sentensi. Kwa hiyo, naomba tumruhusu amalizie sentensi yake, Mheshimiwa Devotha Minja dakika moja.

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Watanzania wanataka kujua kuhusu ndege yao kubwa iliyokuja ambayo ilifanya shughuli zote nchi nzima zikasimama, watu wakaenda kuipokea mpaka kwenye runway wamekaa wanashangilia, iko wapi ndege hiyo, inafanya nini, imeingiza nini toka imeingia hapa nchini?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)