Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Serikali kuonesha kuwa uchumi unakuwa kwa 6.7 mwaka 2018 kutoka 6.2 kwa mwaka 2017, katika kukuza ajira na uboreshaji wa miundombinu na pia imefanikiwa kupunguza mfumuko wa bei katika jamii. Bidhaa na masoko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu hizi bado hazina uhalisia na maisha ya wananchi ambapo bado maisha ni magumu na ajira bado Serikali imeshindwa kutatua kero hii ambayo ndiyo hoja kuu na changamoto kwa vijana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mazingira ya vijana na akinamama wajasiriamali wadogo bado ni magumu katika halmashauri zetu, japo Serikali imejikita katika kuwapa mikopo katika makundi haya, lakini bado marejesho katika vikundi hivi yameshindikana. Kwa hali iliyopo asa sioni kwamba mikopo hii inawasaidia moja kwa moja akinamama kwa sababu urejeshwaji wa mikopo hii kwao bila kuwasimamia, mafunzo, kuwatafutia masoko, miundombinu mibovu imepelekea vikundi hivi kushindwa kufanya biashara na ukosefu wa vifungashio ambavyo ni bora. Matatizo haya ya kimazingira na masoko ni kero kwa wajasiriamali, hivyo Serikali ije na mkakati thabiti kuokoa makundi haya kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vitambulisho vya wajasiriamali wadogo 670,000. Serikali hii pamoja na kuwatambua na kuwaondolea usumbufu wa maeneo ya biashara kupitia Serikali za Mitaa, bado kuna tatizo kwa sababu wajasiriamali wametoa Sh.20,000 lakini mpaka sasa hatuoni kwamba Serikali hii ina nia ya dhati kusaidia kundi hili kwa sababu kundi hili wanalipa kodi, ushuru na huku Serikali iko kimya. Je, ni lini watalimaliza hili kwa wakati?