Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza jitihada za Mheshimiwa Waziri Mkuu za kufua zao la chikichi na kuongeza zao la chikichi katika mazao ya kimkakati nchini. Zao la chikichi litabadilisha uchumi wa Mkoa wa Kigoma na kunufaisha wakulima wa zao hili, lakini pia kufufua zao hili itasaidia kupunguza uingizwaji wa mafuta ya kula kutoka nje ya nchi na badala yake kuchochea uanzishwaji wa viwanda vya kuchakata mafuta ya kula (palm oil) ndani ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la chikichi linahitaji uwekezaji wa miaka mitatu tu lakini mkulima akianza kuvuna anaweza kuvuna kwa zaidi ya miaka nane. Zao la chikichi linaweza kuzalisha bidhaa ya mafuta ya kula (palm oil), sabuni kwa ajili ya matumizi ya nyumbani lakini mashudu ya zao la chikichi yanaweza kutumika kwa ajili ya chakula cha mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mkuu ataendelea kushukuriwa na Wanakigoma kwa kuchochea maendeleo kwa kuhakikisha zao la chikichi linakuwa na tija. Aidha, tunaomba zoezi la upatikanaji wa mbegu za zao la chikichi litiliwe/liongezewe mkazo ili wakulima wapate mbegu za kutosha na mbegu zenye ubora. Mbegu za chikichi zinauzwa shilingi elfu sita kwa mbegu, gharama hii ni kubwa, tunaomba Serikali iweze kuangalia namna ya kurahisisha na kupunguza gharama za upatikanaji wa mbegu za chikichi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kigoma inathamini sana jitihada za Serikali katika kampeni hii muhimu ya kufufua zao la chikichi. Wabunge na wadau mbalimbali tutaendelea kuunga mkono jitihada hizi za Serikali yetu makini.