Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kubwa kwa Serikali kwa juhudi kubwa inayofanya ya usimamizi wa mapato na matumizi katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa. Pongezi kwa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ubunifu wa kutoa vitambulisho vya wajasilimali wenye mitaji midogo. Hili litasaidia kuwatambua na kukuza mitaji yao. Hili ni jambo jema sana kwa Watanzania. Inakadiriwa vitambulisho 670,000 tayari vimetolewa kwa Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali iongoze vizuri katika utoaji wa vitambulisho, sababu kuna wajanja wataanza kujifanya kuwa ni wajasilimali wadogo wadogo ili kukwepa kulipa kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya uchumi inaonekana ni nzuri, hii inatokana na Serikali kusimamia vizuri shughuli za kiuchumi. Kwa mfano, ongezeko la viwanda nchini, kuimarisha ujenzi wa barabara, umeme, maji, Vituo vya Afya na elimu bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali iendelee kutoa elimu kwa Watanzania kuwa, uchumi wa nchi yetu unajengwa na Watanzania wenyewe. Kwa hiyo, kila mtu ana wajibu wa kufanya kazi kwa bidii katika nafasi yake kama ni mkulima alime sana, kama ni mfanyabiashara afanye biashara sana, kama ni mfanyakazi wa kuajiriwa afanye kazi kwa bidii na uaminifu kwa maslahi ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Serikali kwa kusimamia vizuri suala la kupunguza mfumko wa bei kutoka 4.0 (2018) hadi 3.0 Januari, 2019. Hii ni hali nzuri kwa Watanzania. Serikali imesimamia vizuri hasa katika hali ya upatikanaji wa chakula ili kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata chakula cha kutosha na kupunguza njaa katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kwamba kwa kuwa asilimia kubwa ya Watanzania wanategema kilimo, naomba Serikali iimarishe viwanda vya pembejeo hasa viwanda vya mbolea ili wakulima wanunue kwa bei ndogo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na mazao ya biashara, kwa mfano, njegere, njugu, mbaazi, ufuta, maharage, alizeti na njugu. Haya ni mazao ambayo yanawasaidia sana wakulima wadogo wadogo kupata fedha kiurahisi na inasaidia sana kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naunga mkono hoja.