Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kulikuwa na itilafu ya mitambo kidogo, naitwa Stanslaus Mabula, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana. (Makofi/Vigelele)
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie nafasi hii kumshukuru sana Mwenyezi Mungu ambaye ametupa fursa ya kuwepo hapa ndani, lakini nitumie nafasi hii pia kuwashukuru sana wananchi wa Jimbo la Nyamagana kwa kufanya maamuzi sahihi kuwakataa watalii na kuleta wachapa kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, maandiko matakatifu Hosea 4:6 inasema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Kwa hiyo, nataka nikuthibitishie maandiko haya yako watu yanawahusu moja kwa moja. Kwa hiyo, tuliobaki humu tusiwe na shaka kwa sababu sisi tuna maarifa, tunayo kazi ya kulitumika Taifa na Watanzania. Mara zote nimekuwa ninasema tumeanza na Mungu, tutamaliza na Mungu na ndivyo itakavyokuwa. (Makofi)
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuchangia kwanza nimshukuru Mheshimiwa Rais kwa hotuba yake iliyokuwa imejaa na kusheheni mahitaji ya Watanzania. Watanzania wengi wakati wote tumekuwa na subira lakini tumekaa tayari kutegemea hiki ambacho Mheshimiwa Rais sasa anakifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda moja kwa moja kwenye kuchangia hotuba hii yako masuala ya msingi ya kuzungumza juu ya Jimbo langu la Nyamagana lakini juu ya Taifa zima kwa ujumla. Nianze na sekta ya afya. Mheshimiwa Rais amezungumza sana juu ya kuanzisha zahanati kwenye kila kijiji, kituo cha afya kwenye kila Kata, lakini kuhakikisha kila Wilaya ina hospitali na Mkoa una hospitali ya rufaa na Kanda zinazo hospitali za rufaa kwa ajili ya kuhudumia Watanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo ninalotoka mimi la Nyamagana linazo hospitali 12 peke yake kwa maana ya zahanati, lakini siyo Nyamagana tu, ninaamini yako maeneo mengi sana. Kihalisia tunapozungumza kumhudumia mwananchi kwenye sekta ya afya, kuanzia ngazi ya Kijiji, ngazi ya Kata na ngazi ya Wilaya, tunapozungumza kuanzisha hospitali hizi ili zikamilike hospitali yako mambo mengi yanayohitajika, unazungumzia habari ya majengo, watumishi wenye nia njema na thabiti ya kuwatumikia Watanzania, unazungumzia vifaa tiba zikiwemo dawa ili kuhakikisha vyombo hivi na nyumba hizi zinapokuwa tayari Watanzania wenye matumaini na Serikali hii waweze kupata mahitaji yao, tukiamini afya ni suala msingi ambalo linaweza kuwa ni chombo peke yake kwa mwanadamu kinachomfanya awe na uhakika wa kupumua wakati anapopata matatizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaamini Nyamagana inabeba Hospitali ya Rufaa ya Bugando, hospitali hii ni kimbilio la wakazi zaidi ya milioni 14 wa Kanda ya Ziwa, lakini iko based kwenye Jimbo la Nyamagana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, watumishi wanalalamikiwa sana, lakini inawezekana watumishi wanalalamikiwa sana sisi kama Serikali hatujafanya wajibu wetu. Niiombe Serikali ya Awamu ya Tano hospitali yenye vitanda zaidi ya 950 inayotegemewa na watu zaidi ya milioni 14 inaomba bajeti ya takribani bilioni saba kwa mwaka mpaka leo tuko zaidi ya miezi sita imepata milioni 106 peke yake, wananchi wataendelea kulalamika, watumishi wataonekana hawana maana kwa sababu hawatoi huduma zilizobora. Bili ya maji peke yake na umeme kwa mwezi ni zaidi ya milioni 60. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nikuombe sana tuangalie masuala haya kimsingi ili tuweze kutoa huduma. Nyamagana ni Jimbo peke yake lenye kilomita za mraba 256 kilomita 71 zikiwa ni maji lakini hatuna maji ya uhakika ya bomba kwa wananchi wa Jimbo la Nyamagana. Hili ni tatizo na lazima liangaliwe kwa undani. Liko suala la elimu limeshazungumza sana na mimi naunga mkono na wale waliolizungumza. (Makofi)
Suala la miundombinu pia limezungumzwa ziko barabara ambazo hazipitiki, Nyamagana Mheshimiwa Rais wakati amepita ameahidi kuimarisha barabara zinazosimamiwa na TANROAD na zile ambazo alifikiri kwa ahadi yake zitatekelezeka, kutoka Buhongwa kupitia Lwanima, Kata ya Sahwa, Kishiri kuunganisha na Igoma, Fumagira kuunganisha na Wilaya za Misungwi na Magu. Lakini kutoka Nyakato kupita Busweru kwenda Kabusungu, kwenda kutokea Bugombe, Igombe na kuunganisha na Kata nyingine, hii barabara ili iweze kupitika kwa mama yangu Mheshimiwa Angelina kwa sababu haya ni majibu pacha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la miundombinu naomba niseme kwamba liko tatizo kubwa, Serikali hii imejipambanua kukusanya mapato ni lazima tuhakikishe tunapata vyanzo vya mapato. Mwanza ni kituo kikubwa ambacho kinaunganisha mikoa ya Kanda ya Ziwa, nchi za Afrika Mashariki na Kati na Maziwa Makuu hakina airport ya maana ambayo inaweza kuongeza mapato kwa asilimia kubwa. Tuone umuhimu wa kujenga airport ya maana, Internation Airport ambayo itasaidia mtalii anayekwenda Ngorongoro kutokea Arusha akipita kule atokee Serengeti aje aondokee Mwanza, akishukukia Mwanza apite Serengeti aende Ngorongoro aondokee Arusha. Lakini bandari tunaunganisha mikoa zaidi ya sita hakuna bandari ya maana Mwanza hili na lenyewe liangaliwe kwa maana sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, juu ya ukusanyaji wa mapato. Nimuombe Waziri wa TAMISEMI, hakuna siku itakaa Halmashauri hizi ziweze kujitegemea asilimia 50 mpaka 100 maana yake ni kwamba uwezo huo ni mdogo sana lazima tujipange kukusanya mapato.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mabula muda wako umekwisha.
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana naunga mkono hoja asilimia mia. (Makofi)