Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Makame Mashaka Foum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MAKAME MASHAKA FOUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza natoa pongezi kwako kwa kazi nzuri ya kuliongoza Bunge Tukufu. Pia namshukuru Mungu kunijalia afya njema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. Joseph Magufuli pamoja na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Majaliwa Majaliwa kwa kazi nzuri ya kuijenga Tanzania kufikia uchumi wa kati ifikapo 2015. Mwenye macho haambiwi tazama, jitihada za Awamu ya Tano tunaziona, Ilani ya CCM imeweza kutekeleza kama ujenzi wa bandari, ununuzi wa ndege, ujenzi wa madaraja na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu zaidi ni kuhusu uwekezaji sehemu ya uvuvi. Tunayo maeneo makubwa ya uvuvi wa maji baridi na bahari. Kwenye bahari yetu tunao samaki wengi ila tuna upungufu wa vyombo vya uvuvi wa kisasa pamoja na utaalam. Pia tuna upungufu wa viwanda vya kusindika na kuchakata mazao yatokanayo na uvuvi. Naomba Serikali yangu kufanya jitihada za kuwekeza vizuri kwenye eneo hili ili kupunguza tatizo la upungufu wa ajira kwa vijana na kuliingizia pato Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali kufungua vyuo vya uvuvi hasa maeneo ya pwani ili vijana wetu wapate taaluma ya mazao yatokanayo na uvuvi pamoja na kuhifadhi mazingira ya bahari. Yako baadhi ya mazao ya baharini yako hatarini kutoweka kama kovu, kamba na wengine wengi. Hivyo, tuweke mikakati madhubuti ya kuhakikisha tunalinda mazao haya muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante.