Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze hotuba yangu kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia na kunipa afya nikaweza kuchangia hotuba hii muhimu sasa ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kukushukuru wewe binafsi kwa kunipa nafasi ya kuchangia hotuba hii ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa utendaji wake mzuri sana uliotukuka na uliojaa uzalendo mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba yangu hii ninayoitoa Bungeni hapa na pia nitachangia kwa maandishi nitachangia kuhusu hoja moja tu ya uwekezaji ndani ya nchi yangu ya Tanzania. Nimpongeze Rais wangu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kufanya miradi ya maendeleo ya nchi yetu, anamalizia viporo vya tangu Awamu ya Kwanza mpaka sasa Awamu ya Tano. Mungu ambariki sana Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizi kwa Rais, nirudie kumpongeza kwa kuona umuhimu wa uwekezaji Tanzania. Nasema hivi kwa sababu Mheshimiwa Rais ameamua kuiunda Wizara ya Uwekezaji chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, lengo lake likiwa ni kuimarisha uwekezaji nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Dira yetu ya Maendeleo inataka ifikapo mwaka 2025 Tanzania iwe imeshafika kuwa nchi ya uchumi wa kati (middle income country). Nchi haitaweza kufikia nchi ya uchumi wa kati bila ya kuwa na viwanda vya kutosha. Rais wetu amechukua hatua nzuri sana
kumteua Waziri anayesimamia Uwekezaji chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, ambako vilevile tuna Kituo cha Uwekezaji (Tanzania investment Centre) ili kuratibu vizuri juhudi zote za uwekezaji kutoka ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili alilolifanya katika mikakati yake ya kuboresha uwekezaji ni pale alipomtaka kwamba mwaka 2019 kuwa ni mwaka wa uwekezaji Tanzania. Alitoa tamko hili mbele ya Mabalozi wote wa nchi za nje wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania. Tamko hili la Rais ni la Kitaifa na ni la Kimataifa. Mheshimiwa Rais kutoa tamko hili la kuutambua mwaka 2019 kuwa mwaka wa uwekezaji amewatuma Mabalozi wa nchi za nje kualika nchi zao kuja kuwekeza nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuchangia uwekezaji nchini nikisema yafuatayo. Tanzania tunalima pamba kwenye Mikoa mikuu minne ambayo ni Simiyu; Shinyanga; Mwanza na Geita. Simiyu peke yake inaongoza kwa kulima pamba zaidi ya 40% ya pamba yote inayolimwa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuiangalie Tanzania kwenye kilimo cha pamba ndani ya Afrika na ulimwenguni. Tanzania kwa kulima pamba inashika nafasi ya 8 kati ya nchi 30 za Afrika zinazolima pamba. Tanzania inashika nafasi ya 22 duniani kati ya nchi 77 zinazolima pamba. Katika hali kama hiyo, Tanzania Afrika na duniani tunalima pamba. Pamoja na Tanzania kuwa nafasi nzuri sana katika kilimo cha pamba lakini kuna tunachokosea na hivyo hatupati faida kubwa kiuchumi kutokana na zao hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natumia muda wote nilio nao kuishauri Serikali kwamba tutumie zao hili la pamba kupata wawekezaji wa textile industry (viwanda vya nguo). Mheshimiwa Rais alipoteua Waziri wa Uwekezaji chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, lengo lake ni kwamba anataka kuboresha uwekezaji nchini. Mimi ni Mbunge mkongwe, namfahamu Mheshimiwa Waziri aliye na dhamana ya Uwekezaji, Mheshimiwa Angellah Kairuki, nimshauri afanye kila jitihada kuhakikisha zao la pamba linapata wawekezaji wa textile industry.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kidogo niongelee nchi ya Bangladesh. Nchi ya Bangladesh ipo katika Bara la Asia. Ni nchi ndogo, ina eneo la kilomita za mraba takribani 148,000. Pamoja na udogo huo, Bangladesh ina population ya watu wapatao milioni 165. Nalinganisha Bangladesh na nchi yangu Tanzania. Tanzania ukiilinganisha kieneo na Bangladesh ni kubwa ina eneo za kilomita za mraba 945,087 na kulingana na sensa ya mwaka 2017, population yake ni milioni 57.31. Nimependa kuilinganisha Bangaladesh na Tanzania kutokana na jinsi ambavyo nchi hii ndogo ya Bangaladesh….