Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi anazofanya kwa umahiri mkubwa. Namuombea Mungu azidi kumtia nguvu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazo ahadi za Mheshimiwa Rais katika Jimbo la Mbulu Vijijini ambayo ni barabara ya lami toka Mbulu – Haydom - Sibiti. Naomba itengwe fedha ya kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami kutoka Haydom - Mbulu maana hatuna kabisa lami katika Jimbo la Mbulu Vijijini. Kwa kutekelezwa kwa ahadi hii ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli itakuwa imetatua kero kubwa ya wananchi ya kushindwa kufika katika Hospitali ya Haydom. Pili, kwa kufanya hivyo mtakuwa mmetekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne na Tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaipongeza Serikali kwa ujenzi wa Kituo cha Afya Dongobesh. Tunaomba tupewe fedha za kujenga Kituo cha Afya Maredadu maana wananchi wameshajenga katika hatua ya mwanzo ya ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo la kutomalizika kwa miradi ya maji katika Jimbo la Mbulu Vijijini, mfano mradi wa Arri – Harsha na Tumati Mungasharq. Tunaomba msukumo wa Serikali katika miradi hii ya maji. Nashauri pawepo na Mamlaka za Maji za Mikoa ili ziweze kuisimamia miradi ya wilaya kwa ukaribu zaidi na certificate zilipwe kwa wakati.