Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa hotuba yake nzuri sana ambayo imeonesha mafanikio mengi sana ambayo yamefanyika nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kutoa elimu bila malipo. Changamoto nyingi zimejitokeza kama upungufu wa vyumba vya madarasa, madawati, vyoo, nyumba za walimu, walimu na vitabu vya kujifunzia na kujifunza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikali kwa kuboresha afya za Watanzania nchini. Upande wa afya Jimboni kwangu kuna baadhi ya changamoto kama vile upungufu wa wahudumu katika vituo vya afya na zahanati zetu. Pia katika vituo vyetu vya afya hatuna mashine hata moja ya picha ya X-ray na baadhi ya vifaa muhimu vya uchunguzi wa afya ya binadamu. Pia kuna upungufu mkubwa wa vitambulisho kwa wazee kwa ajili ya matibabu bure kwa wazee. Ni wazee 100 tu kati ya 6,000 ambao wana vitambulisho nchini, sasa hawa wazee 5,000 watapatiwa vitambulisho hivyo lini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikali kwa kuboresha baadhi ya kero kwa upande wa madini. Kwa upande wa Jimbo la Nyang’hwale bado kuna kero kubwa kwa wachimbaji wadogo kwa kutopimiwa maeneo yao na kupatiwa leseni za uchimbaji. Maeneo hayo ni Bululu, Ifugandi, Isonda, Isekeli, Lyulu, Nyamalapa, Kasubuya, Rubando, Iyenze, Shibaranga na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kupunguza kero ya maji vijijini na mijini. Kwa upande wa Jimbo langu la Nyang’hwale, kuna mradi mkubwa toka chanzo cha Ziwa Viktoria kutoka Nyamtukuza, Kakora, Kitongo, Ikangala, Kharumwa, Iyenze na Bukwimba. Mradi huu umeanza tangu 2014 hadi leo 2019 hata tone moja la maji halijatoka na kusuasua kwa wakandarasi wanadai Serikali haijawalipa fedha. Nataka kujua tatizo liko wapi, ni Serikali kutowapa malipo au wakandarasi ni matapeli?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikali kwa kuboresha miundombinu ya barabara kwa viwango vya lami na changarawe. Kwenye Jimbo la Nyang’hwale kuna ahadi za viongozi wa nchi, kuna Rais wa Awamu ya Nne kuhusu ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami toka Kahama - Nyang’holongo – Bukwimba – Kharumwa – Nyijundu – Busorwa – Busisi. Pia Rais wa Awamu ya Tano naye aliahidi, je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuunga mkono hoja hii.