Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimwa Mwenyekiti Ahsante, kwanza naomba nichukue nafasi hii kuipongeza Wizara ya TAMISEMI, lakini pia kuwapongeza Mawaziri wote pamoja na Serikali nzima kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya kuhakikisha kwamba wanalitoa Taifa letu kwenye uchumi wa chini na kulipeleka kwenye uchumi wa kati ifikapo 2025. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa speed ambayo inaonekana, sina mashaka kabisa, 2025 kama tutakuwepo, basi tutakuwa wote tunaona tumefika kwenye uchumi wa kati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, sana naomba nichangie mchango wangu kwenye upande wa TARURA. TARURA kama walivyosema wenzangu, inapewa asilimia 30, lakini TARURA ina kilometa 130,000 na TANROAD wana kilometa 30,000. Sasa TARURA wana kuwa hawawezi kufanya kazi zao vizuri kwa sababu bajeti ni ndogo sana.

Mheshimiaw Mwenyekiti, kwa sababu sheria hizi zilivyokuwa zinatungwa zamani, ilikuwa bado hawajaunganisha zile barabara mkoa kwa mkoa, lakini kwa sasa hivi watu wa TANROAD wameshaunganisha barabara zao mkoa kwa mkoa na nyingine wameshaunganisha wilaya kwa wilaya. Kwa hiyo, naomba niishauri Serikali iweze kubadilisha sheria ili watu wa TARURA waweze kuongezewa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa kuna tatizo kubwa sana hasa sisi Wabunge tunapoenda kufanya mikutano yetu. Tunaenda kufanya mikutano yetu tunaahidi wananchi kwamba hapa sehemu hii itajengwa barabara na ndivyo tunavyokuwa tumeaambiwa na watu halmashauri pia na watu wa TARURA wanakuwa wamepanga bajeti yao, lakini ukiangalia sana unakuta kwamba TARURA wana matatizo ya bajeti. Dar es Salaam kuna matatizo makubwa ya barabara, ukiangalia barabara za Jimbo la Segerea tuna barabara moja ambayo iko Kata ya Kimanga, sasa hivi hiyo barabara inajengwa kwa miaka mine, lakini tatizo kubwa ni bajeti, TARURA haina pesa ya kumalizia ile barabara iweze kumalizika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tuna barabara nyingi mfano kama Jimbo la Ukonga barabara ziko kwenye hali mbaya, barabara ya Pugu, barabara ya Majohe, Barabara ya Kitunda – Banana, barabara zote hizo zinasubiri TARURA, lakini TARURA hawana bajeti walipanga mwaka jana hizo barabara zitajengwa, lakini haziwezi kujengwa kwa sababu bajeti hakuna. Sasa nataka nishauri Serikali kwamba hii sheria ibadilishwe, TARURA waongezewe fedha ili waweze kupanga kuendana na mipango yao wanayoipanga, lakini kama tutaendelea hapa kwamba TARURA watakuwa wanapewa asilimia 30, haiwezekani, itakuwa mipango yetu ya kusema kwamba tunajenga barabara Fulani, barabara hazitajengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ni mbaya sana ukiangalia Kata ya Kipawa pale tuna terminal one, two na three tunategemea kufungua airport ya kisasa terminal three, lakini opposite na hiyo airport barabara ni mbovu sana, sasa tunasema kwamba tunakaribisha wawekezaji, wanapokuja hapa inatakiwa pia miundombinu iwe mizuri. Sasa mwekezaji anatoka tu airport anakutana na barabara mbovu, kwa kweli hiyo inamkatisha tamaa. Niwaombe sana tuangalie hili suala la kuongeza fedha kwenye Mfuko wa TARURA. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ninachotaka kuongelea ni kuhusiana na ushirikiano wa hizi taasisi mfano TARURA, DAWASA, Wizara ya Maji pamoja na TANESCO, unakuta barabara imetengenezwa, TARURA wametengeneza barabara baada ya miezi miwili DAWASA wanakuja wanachimba wanapitisha miundombinu yao, mashimo yale yanakaa miezi hata sita hayajawahi kuzibwa. Sasa huu pia ni upotevu wa mapato ya Serikali kwa sababu baada ya kuchimba wanakuja wanaziba ni kutengeneza vitu mara mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kama inawezekana, kama kuna mradi ambao unafanyika sehemu Fulani, taasisi hizi za Serikali ziweze kuwasiliana ili wakae waone kwamba hapa tunapitisha mradi fulani, waweze kuweka miundombinu yao kwa pamoja, sio barabara imejengwa TANESCO wamekuja, DAWASA wamekuja TANESCO wanakuja ooh hapa tunapitisha nguzo, kwa hiyo inabidi tubomoe barabara. Naomba sana hilo jambo lifanyiwe kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kuongelea ni kuhusiana na suala la elimu. Tumekuwa tuna tatizo kubwa sana, watoto wetu wanapoanza shule darasa la kwanza. Sasa kama sasa hivi mwaka jana wamemaliza wanafunzi 22,285, mwaka huu wameingia wanafunzi 44,656, tunajua hawa wanafunzi wameingia na sasa hivi Serikali imeleta utaratibu kwamba wanafunzi wote wanakuwa kwenye system. Sasa Serikali inashindwajwe kujua kwamba mwaka 2020 mwezi wa Kwanza wataingia watoto fulani ili sasa tusije tukaanza yale mambo ya zima moto. Kwa hili kwa kweli nichukue nafasi hii kuwapongeza sana viongozi wa Dar es Salaam, Mkuu wangu wa Wilaya Sophia Mgema, Mkurugenzi wangu pia na Mkuu wa Mkoa wamekuwa wakifanya kazi kubwa kuhakikisha madarasa ya zimamoto yanajengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa sababu tusiwe tunafanya kazi kwa zimamoto tuna hesabu sasa hivi za watoto ambao wameanza shule ya awali, lakini pia tuna hesabu ya watoto ambao wanaanza darasa la kwanza, tunajua kwamba baada ya muda gani watoto watamaliza shule. Sasa kuepukana na haya matatizo ya kufanya kazi kwa zimamoto tuiombe sana TAMISEMI iweze kuandaa miundombinu na tukisema miundombinu hatusemi tu miundombinu ya madarasa tunahitaji tupate miundombinu ya vyoo, kama sasa hivi kuna watoto wengi wanakuwa kwenye shule moja tunahitaji tupate miundombinu ya vyoo lakini tupate miundombinu mingine ambayo itawawezesha wale watoto waweze kusoma vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niongelee kuhusiana na zahanati au vituo vya afya. Kwanza nichukue nafasi kumshukuru sana Mheshimiwa Jafo kwa kuleta milioni 500 kwenye kituo chetu cha Plan International lakini nataka tu nikwambie Mheshimiwa Jimbo la Segerea lina wakazi milioni moja elfu kumi na sita, tuna kituo kimoja tu cha afya. Sasa kwa kuwa na kituo kimoja tu cha afya kwa jimbo zima kama lile na lenye wakazi kama wale bado tuna changamoto kubwa. Tunaomba tupate kituo kingine na tuna maeneo makubwa mfano kama zahanati ya Seregea ina eneo kubwa sana la kujenga kituo cha afya. Pia ukienda Kinyerezi pia kuna zahanati pia ina eneo kubwa la kujenga kituo cha afya na Tabata. Tungeomba tupate hivi vituo vya vinne ambavyo vinaweza vikatusaidia katika Jimbo la Segerea kwa sababu mambo mengine yote yanaweza yakaishia kwetu kwenye Jimbo la Segerea kabla hatujaenda Amana.