Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipatia fursa ya kuchangia Wizara hizi muhimu katika maendeleo ya Watanzania. Awali ya yote, niwashukuru Waheshimiwa Mawaziri kwa wasilisho zuri, masilisho lenye vielelezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siwezi kuchukua muda mwingi kuzungumzia hilo kwa sababu natoka kijijini kama ni shule nimeziona. Wale waliosafiri kwenda kwetu, Kaitu Kaila kuna misemo inasema mtenda kazi ndiye huleta kazi, mtenda kazi aliyeamua watoto wote waende shule ndiyo aliyeleta kazi. Kwa hiyo, ukiona watoto wako wengi shule hawana madarasa ni kwa sababu mtenda kazi amesema wote waende shule na nina imani mtenda kazi atawafuata kule wale watoto atawapatia madarasa, vyoo na mambo yatakwenda mbele. Kama mtenda kazi asingesema muende shule wala msingewaona na hali ingekuwa siyo nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali miundombinu ya shule inayotakiwa ni mingi, pamoja na jitihada zetu za kujenga miundombinu Serikali itoe vivutio kwa sekta binafsi iingie kwenye kuendesha shule. Vyumba 85,000 Serikali hatutavimaliza kesho sasa sekta binafsi ihamasishwe, ipewe vivutio vya kila namna kusudi na wao waingie kwa sababu vijana hawa hawatasubiri, waweze kwenda kwenye shule hizi walipe pesa kidogo kidogo. Hilo la elimu nimelimaliza na nishukuru kwa kazi zote ambazo mmefanya kwenye Jimbo langu la Muleba Kaskazini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la afya. Napokuja kwenye afya niwashukuru wananchi wangu wa Jimbo la Muleba Kaskazini lakini niwashukuru wadau wangu wa maendeleo, katika Jimbo langu tumetengeneza zahanati 12. Unajua mtoto anapoanza kufyeka shamba mzazi unamwekea msingi, naiomba Serikali katika maeneo yangu yenye maeneo hatarishi kama Kisiwa cha Bumbile ambako kuna shughuli za uvuvi na kuna mapato mengi tunaomba tuwekewe kituo cha afya. Kuna sehemu za low lands upande wa Magharibi mpakani na Karagwe, sehemu za Ngenge tungeweka kituo cha afya kuwasaidia watu wa eneo lile ambao wao wanatembea siyo chini ya kilometa 30, 40 kuweza kupata huduma ama kwenda Muleba au Bukoba Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napomaliza hilo nizungumzie suala la TARURA, tofauti na wenzangu waliozungumza mimi sitawaliwi na asilimia. TARURA mnapojijenga upya mfanye tathmini ya uhalisia wa barabara zenu mlizo nazo na sisi Wabunge tupewe fursa ya kutengeneza Mfuko wa Barabara za Vijijini. TARURA amepata ngapi, TANROADS amepata ngapi haina tija, tija itokane na kutenga mfuko wa kuweza kutengeza barabara. Kimsingi hata mgao huu unaofanyika unakuta Wilaya moja anapewa pesa nyingi mwingine anapewa kidogo bila kuzingatia uhalisia wa barabara. Kwa hiyo, solution ni mfuko yaani shida ya jirani yako isikufanye wewe ufurahi, TANROADS apate pesa za kutosha na TARURA apate pesa za kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la mikopo wanayopewa vijana na akina mama na hili nizungumze nikihusisha na shughuli ya Wizara hii ya TAMISEMI kuhusu suala la viwanda. Nakumbuka katika kitabu kimoja nimewahi kusoma kinachozungumzia mwongozo wa ujenzi wa viwanda katika Tawala za Mikoa na Vijijini kinaeleza watu weledi na maeneo yako kule vijijini. Kwenye vitabu inaonyeshwa kwamba shilingi bilioni 62 zinatumika kuwapa watoto na akina mama, nashauri Serikali mngechukua shilingi bilioni 62 sehemu yake mkanunua matrekta, kwa sababu vijana wengi wako vijijini wapeni matrekta, muwape viwanda badala ya kuwapa shilingi laki mbili mbili, wanakwenda kugawana umaskini. Nichukue fursa nikushukuru Mheshimiwa Jafo namna unavyoendelea kuhamasisha viwanda. Mimi niliacha viwanda 3,540 nimesikia wewe una 4,000, unanitia moyo, endelea kuhamasisha viwanda. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la watumishi, nichukue fursa hii kuiomba Serikali kwenye sekta ya afya na elimu tuwatafutie watumishi, pelekeni watumishi kule. Mimi chumba cha darasa hakinipi shida, unaweza kutengeneza makuti ukaweka pale. Nimewahi kulisema na nalisema tena, Muadhama Laurean Cardinal Rugambwa yeye alianzisha…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)