Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Hassanali Mohamedali Ibrahim

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiembesamaki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE.IBRAHIM HASSANALI RAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nimshukuru kaka yangu kwa imani yake aliyonipa hizo dakika tano nichangie, kwa hiyo zitakuwa ni kumi, Mwenyezi Mungu amzidishie. Pia nikushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia hotuba za Mheshimiwa Waziri kaka yangu Mheshimiwa Jafo na Mheshimiwa George Mkuchika katika hotuba zao. Kabla sijaendelea huko mbele nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa pumzi zake mie kusimama hapa na kuweza kuzungumza mambo mawili matatu ambayo yatasaidia kueleza changamoto zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza na Wizara ya TAMISEMI, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Jafo kwa kazi kubwa anayoifanya. Kwa kweli naweza kusema ni Waziri mwenye kiwango, nikisema Waziri mwenye kiwango kwamba ni Waziri ambaye kwa kweli ameleta matumaini mapya kwa wananchi na kwa Serikali yetu hii ya CCM. Nampongezasana Mheshimiwa Jafo pamoja na wenzake, Manaibu wake kwa kazi kubwa wanayoifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka vilevile nizungumzie changamoto ambazo zinatokana na hii Wizara. Kwanza kabla sijakwenda huko niwapongeze Wakuu wa Mikoa, kwa sababu Wakuu wa Mikoa kwakweli kwa awamu hii wanafanya kazi nzuri na wanasimamia mapato ya halmashauri, lakini baadhi ya halmashauri hawajafanya vizuri katika ku-collect zile ten percent ya vijana akinamama na watu wenye ulemavu. Kwahiyo, naomba sana Wakuu wa Mikoa wawe kidogo wakakamavu na wawafuatilie Wakurugenzi wao kwasababu tunayo taarifa kwamba halmashauri nyingi zimekuwa hazifanyi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ambazo nataka kuzungumzia hapa kwanza hii ya ten percent ambao kwa kweli baadhi ya Wakurugenzi wanakuwa hawazikusanyi hizi pesa zinavyotakiwa na vilevile wanazitumia kwa matumizi mengine ambapo hii ten percent ya vijana, akinamama na walemavu, tumepitisha hapa Bungeni ikawa ni sheria mama kwamba zitumike katika mambo tuliyokusudia. Kwahiyo, ningeomba sanaWakurugenzi hili suala la ten percent, huu ndiyo uhai wa wananchi wetu maskini ambao wanategemea hii asilimia kumi kufanya miradi yao ambayo inayaendeleza mbele maisha yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine Mheshimiwa Waziri nikija kwenye suala la usafiri waDART, hili limekuwa janga katika Jiji la Dar es Salaam. Nasema janga kwa sababu nimeshuhudia na nimepata malalamiko mengi sana kwa wananchi wetu kwamba mabasi hayatoshi, mabasi mengi yameharibika na vilevile pale Kimara pamekuwa watoto na akinamama wanavyobanwa hata kuvuta pumzi wanashindwa wengine wanarudi nyumbani hawaendi makazini. Sasa hili suala la DARTnamwomba sanaMheshimiwa Waziri alivalienjuga, kwa kweli nikimpelekea picha ambazo ninazo kwenye simu zangu atawaonea huruma akinamama na watoto wanavyobanwa, yaani wamebanwa na wengine wanakanyangwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa haya matatizo ya DARThao Wapinzani wanaidakia sana hii, kuikemea Serikali na kuitukana Serikali yetu ya CCM, hiyo ndiyo imekuwa ajenda yao wapinzani, lakini hawajui kwamba matatizo haya yanawahusu na wao vile vile siyo watu wa CCM tu. Kwahiyo, namwomba Mheshimiwa Jafo suala la DARTna kama huyu mwekezaji amefeli hawezi basi aniambietu Mheshimiwa Raza hebu tutafutie mwekezaji mwingine, nitamtafutia mwekezaji mzuri sana ambaye ataondoa matatizo haya ya usafiri wa mabasi Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwa mzee wangu KapteniGeorge Mkuchika, nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, ni kaka yangu, ni mzee wangu, nimpongeze kwa hotuba yake nzuri ambayo haina mashaka. Sisi nimashahidi wa Tanzania, utawala huu wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli hauna doa hata zeropointone percent. Nataka niwaambie Wapinzani kwamba huu utawala bora uliokuwa Tanzania, tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa Mungu alivyompa imani Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa mambo anayoyatenda, lakini kuna nchi huwezi ukasema jambo lolote la ubaya wa yule mfalme ambaye anaongoza katika nchi ile, utapotea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa leo Tanzania hii, watu wana fursa ya kuzungumza, wanafursa ya kusema, wanafursa ya kutembea, leo mwisho tunakuwa hatuthamini utawala bora ambao unaongozwa na Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli. Kwa kweli naweza kusema kwamba, Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli amekuwa ni mfano katika Afrika na sasa hivi katika Afrika sisi tupo post ya juu kabisa katika nchi ambayo ipo amani katika nchi hii yaani tujipongeze sisi Wabunge wote kwamba Tanzania ipo juu katika amani. Isitoshe katika Afrika tu hata katika nchi za Afrika Mashariki na kati we are top number one katika amani. Kwahiyo, hii peke yake inasadikisha kwamba kweli utawala bora uliokuwepo na amani ipo, ungekuwa utawala bora si mzuri, basi na amani isingekuwepo, ingetoweka. Kwahiyo,Mheshimiwa Waziri, MheshimiwaKapteni George Mkuchika, namwambia aendelee hapo hapo na kama kuna msumeno aendelee, lakini tuweke nchi katika hali ya nidhamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile niwapongeze ndugu zangu wa TAKUKURU, wameweza kufanya kazi kubwa sana ya kuwapeleka mahakamani mafisadi wakubwa ambao walikuwa wanajulikana mapapa wa nchi hii. Nataka nimwambie Mkurugenzi wa TAKUKURU, Diwani Athman kwa sababu namwamini na pale alipowekwa na Mheshimiwa Rais kwa sababu naye kamwamini, kwahiyo Ndugu Diwani Athuman apige kazi, asiogope sura ya mtu, bado kuna mafisadi wamefichika ndani ya pazia, wamefilisi nchi hii, kwahiyo Mheshimiwa Waziri nataka ashirikiane na huyu Mkurugenzi wetu wa TAKUKURU ili aweze vile vile kuwafichua wengine ambao wamefilisi nchi hii na kutufikisha hapa tulipofika.

Mheshimiwa Mwenyekiti,kwahiyo nampongeza sana. Kwa kweli rushwa imeondoka Tanzania sivyo kamatulivyokuwa miaka ya nyuma, sasa hivi nidhamu imerejea katika kazi. Rushwa ndogo ndogo ipo bado, lakini na hakika chini ya Wizara yaMheshimiwa George Mkuchika na hizo rushwa ndogo ndogo nazo zitaondoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hayo machache, nafikiri nimetumia muda wangu dakika kumi kama ipasavyo, nikushukuru kwa kunipa nafasi na naiunga mkono Wizara hii hundred percent. Pia Wizara ya Mheshimiwa Jafo naiunga mkono hundred percent.Mwenyezi Mungu ampe afya na umri Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Amini.(Makofi)