Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Lushoto lina zaidi ya shule za msingi 33 nasekondari 26 za Serikali, lakini katika shule hizi kuna changamoto nyingi kama:-

(i) Ukosefu wa nyumba za walimu wa shule ya sekondari na msingi;

(ii) Ukosefu wa hostel katika sekondari zetu;

(iii) Fedha za ukarabati wa shule za msingi za Kilole, Kwemashai, Malibwi, Kwembago, Ngulwi, Ubiri, Milungui, Kwemakame na Yogoi;

(iv) Kumalizia maabara zilizojengwa kwa nguvu za wananchi;

(v) Upungufu wa walimu wa shule ya msingi na sekondari;

(vi) Walimu kutolipwa posho zaonakuwekewa miundombinu rafiki;

(vii) Watumishi kutopandishwa madaraja; na

(viii) Ukosefu wa fedha za kumalizia maboma yote ambayo hayajakamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kuwasilisha.