Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa pongezi za dhati kwa Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuwaletea maendeleo wananchi. Waziriwa TAMISEMI, Mheshimiwa Selemani Jafo,Naibu Mawaziri wake, Katibu Mkuu na Naibu Makatibu Wakuu wanafanya kazi iliyotukuka na kwa ufanisi na maendeleo yaoonekana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri George Mkuchika na timu yake wamejitahidi kuweka hali sawa ya utawala bora na kutoa vibali vya ajira na kujaza nafasi za utumishi za kada mbalimbali hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu asilimia 10 ya mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu inayotoka ndani ya mapato ya Halmashauri zetu, kazi hii inaendelea ndani ya Halmashauri zetu kwa kiwango tofauti. Tunaomba Waziri, Mheshimiwa Jafo kwa umahiri wake kuona umuhimu wa kutoa usafiri wa pikipiki angalau kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Vijiji na Mitaa na ngazi ya Wilaya (Halmashauri) na Mkoa wapatiwe magari kuliko kutegemeahurumaya Wakurugenzi wao. Pia tunaomba ajira ya Maafisa Maendeleo ya Jamii, kwani wana kazi kubwa ya kuelimisha wananchi hasa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kuunda vikundi vya ujasiriamali ili waweze kupata mikopo.