Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Eng. Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE.DKT. CHRISTOPHER K. CHIZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri na Wasaidizi wake wote kwa hotuba nzuri. Nimesikiliza hotuba kwa makini sana, imenikumbusha mambo kadhaa yanayohusu mawasiliano Serikalini Standing Orders na hata Financial Orders (Stores Regulations) nakadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya LAAC.Katika kupitia hoja za ukaguzi za CAG zinazohusu Serikali za Mitaa na baada ya ziara ya kukagua miradi katika Halmashauri 12, nimejiridhisha kwamba Serikali inaweza kupunguza hoja za ukaguzi kama watumishi wanaopewa dhamana kuwa Maafisa Masuuli (DEDs) wangepata uelewa wa shughuli za Serikali.Watendaji wengi wakiwemo Wakuu wa Idara wapo wasiojua kanuni na taratibu za uendeshaji shughuli za Serikali. Baadhi yao hata hawajajua nini maana ya uwajibikaji na utunzaji wa siri za Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kamani gharama kuwapeleka viongozi wa Serikali kufundishwa katika Chuo cha Utumishi Serikalini, nashauri Chuo na Maafisa Waandamizi wa Serikali wafanye semina hizo katika maeneo ya kazi. Athari ya kuwa nawatumishi wasiojua Miiko ya Utumishi (The DOS and DONTS) inaweza kuigharibu Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.