Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI:Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa George Huruma Mkuchika, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) pamoja na Naibu Waziri na Katibu Mkuu kwa kazi kubwa wanayoifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, naombawaangalie suala la watumishi wa afya walioajiriwa kihalali na Serikali baada ya kuwalegezea masharti ya ajira na ambao waliondolewa kwenye utumishi wa umma kwa kukosa sifa ya kumaliza kidato cha nne. Ni vyema watumishi hao wakarudishwa kazini ama kustaafishwa na kulipwa mafao yao. Baadhi ya watumishi hao wapo wa kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo ambao wameleta malalamiko yao ya kutotendewa haki kwa Katibu Mkuu Dkt. Laurean Ndumbaro na nakala ya malalamiko hayo nilimkabidhi Mheshimiwa Dkt. Mary M. Mwanjelwa, Naibu Waziri.Watumishi hao wamekuwa wakipoteza nauli mara kwa mara kuja Dodoma kufuatilia majibu ya malalamiko yao na hivyo kujiongezea machungu na umaskini. Naomba suala lao lishughulikiwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimekuwa nikipokea vilio vya baadhi ya watumishi wa Serikali hususan wa TAMISEMI (Makao Makuu) wanaolalamikia maslahi duni. Wanasema wenzao wa kada moja walioajiriwa kwenye Taasisi za Serikali wanapata mishahara minono wakati wao walioajiriwa TAMISEMI mishahara wanayoipata haikidhi kabisa mahitaji ya msingi na hivyo kujikuta na madeni lukuki na kuendelea kuishi kwa kuombaomba. Wameniomba nifikishe kilio chao kwa Mheshimiwa Rais kupitia Wizara hii yenye dhamana na mishahara ya watumishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia 100 na naomba kuwasilisha.