Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi kwa Mheshimiwa George Mkuchika, pia Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa kwa hotuba nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, natoa pongezi kwa Mkurugenzi wa TASAF kwa kazi nzuri ya kusaidia kupunguza makali kwa wananchi walio masikini, angalau kwa sasa wanakula milo mitatu, watoto wanaenda shule na wanawake wengi wamepeleka watoto Clinic.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfumo wa awamu ya tatu isaidie walengwa ambao wamefanikiwa kujikwamua kwa maendeleo ili wale ambao hawakuingia awamu ya kwanza na ya pili, kutoa nafasi nao wawezeshwe. Pongezi kwa kutafuta wafadhili wenye mikopo nafuu ili kusaidia maendeleo kutokana na bajeti kuwa finyu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni MKURABITA. Serikali iongeze bajeti ya maendeleo ili kupunguza migogoro ya ardhi, pia wananchi waweze kupata hati za kimila na kuweza kukopa. Serikali iendelee kufuatilia fedha za maendeleo za mwaka 2018/2019 ili zitolewe kabla ya Juni, 2019 zifanye kazi iliyokusudiwa. Hata hivyo, naomba MKURABITA ibuni jinsi ya kupata wafadhili kwa kuandika michangonuo ya mikopo yenye riba nafuu kama walivyofanya TASAF kwa kutegemea Serikali hawajafikia malengo waliyokususidiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara iangalie jinsi ya kumaliza suala zima la watumishi wanaokaimu kwenye ofisi mbalimbali, kupandisha madaraja kwa wale wanaostahili, uhakiki na madeni ya watumishi yafanyike haraka, vibali vya ajira vitoke haraka kwenye Wizara mbalimbali kutokana na wahitaji ili watumishi waajiriwe hasa katika huduma ya afya na elimu.