Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Serikali Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri na Makatibu Wakuu kwa kazi nzuri wanazozifanya za ujenzi wa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, NEMC; naomba Serikali waangalie utendaji wa NEMC kwani washauri wanachukua fedha nyingi kuliko Serikali. Waangalie mradi gani unahitaji upembuzi wa muda mrefu na mengine kama imeshapitishwa na Halmashauri NEMC wapitishe kwa haraka. NEMC na taasisi nyingine kama EWURA na wengine wakae pamoja na kutafuta njia nyepesi ya kuwasaidia wawekezaji wa mafuta (naweka maslahi wazi ni mdau). Badala ya kulipa malipo makubwa mara moja, nashauri katika kukuza na kuendeleza uwekezaji waweke tozo ambazo zinaweza kulipwa kila mwaka, hii itasaidia hata wawekezaji wadogo kuweza kumudu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mifuko ya plastic; naipongeza Serikali kwa uamuzi wake wa kupiga marufuku kwani mazingira yetu yaliharibika vibaya kutokana na mifuko kujaa ardhini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Muungano; naipongeza Serikali kwa kujitahidi kutatua kero za Muungano kwa kiasi tulichofikia inatia moyo sana. Tudumishe Muungano wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.