Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, napenda kuunga mkono hutuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani, naishauri Serikali izingatie ushauri uliotolewa katika hotuba ile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala uchafuzi wa mazingira na kukosekana kwa usimamizi mzuri unasababisha uharibifu wa mazingira. Nani asiyejua uidhinishaji/usajili unaofanywa wa viwanda ambavyo ni hatari kwa mazingira yetu? Hivyo basi, pamoja na kauli ya Waziri Mkuu kupiga marufuku utumiaji wa mifuko ya plastiki, je, kauli hiyo imeenda sambamba na ufungaji viwanda vinavyozalisha mifuko hiyo? Je, kauli ya Waziri Mkuu inaenda sambamba na utoaji wa elimu kwa wananchi hasa vijijini? Nina mashaka makubwa na faini/ vifungo watakavyopata wananchi hasa vijijini. Naishauri Serikali itangaze kufunga viwanda vya utengenezaji mifuko hiyo mara moja na elimu itolewe kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ukataji wa miti unakithiri kila mwaka na hakuna jitihada za upandaji miti hali ambayo inasababisha mabadiliko makubwa ya hali ya hewa. Serikali iweke mkazo katika upatikanaji wa gesi na umeme vijijini na mijini kwa matumizi ya viwanda, magari na majumbani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nashauri Serikali ipeleke miradi ya ufugaji nyuki kwa wananchi vijijini. Ahsante.