Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana nami kuchangia kwenye Wizara hii nyeti na muhimu ya Muungano na Mazingira. Wilaya yetu ya Kilosa ni Wilaya Kongwe sana hapa nchini; na kwa kweli changamoto kubwa sana tunayoipata kila mwaka ni mafuriko ya mara kwa mara ambayo yanasababisha vifo, uharibifu mkubwa wa mashamba, mali na miundombinu mbalimbali katika Wilaya ya Kilosa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu kubwa ya mafuriko hayo ni kupasuka kwa bwawa la Kidete ambapo mvua zinaponyesha kidogo tu yanamwagika kwa wananchi lakini pia kupoteza ulekeo wa mto Miyombo ambao ni mto unaopita kwenye kata nyingi za Wilaya ya kilosa yenye Majimbo ya Kilosa kati na Mikumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaiomba sana Serikali itusaidie pesa ili kujenge bwawa hili muhimu la Kidete kwa kuwa Waziri wa Maji alishafanya ziara na kuahidi kuwa pesa zimeshatengwa na wapo kwenye mchakato wa kumalizana na mkandarasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mto Miyombo tunaomba sana tujengewe tuta katika Kata ya Masanze iliyopo Jimbo la Mikumi ambapo kwa ujenzi huu wa tuta ni muhimu sana na utasaidia sana kuzuia maji yasiende kwenye makazi ya wananchi na kuepusha maafa ambayo yanatokea mara kwa mara kwenye kata hii pamoja na Kata Magomeni na kuleta maafa makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaiomba sana Serikali kuchonga kingo za Mto Miyombo hasa kwenye maeneo ya Kata ya Kilangali ili kuzuia maji kuingia kwenye maeneo ya wananchi (makazi na mashamba yao) na kuyaharibu vibaya sana kutokana na mto huu kupoteza uelekeo mara kwa mara kwa kuzidiwa na maji mengi ambayo yanatiririka kwa wingi sana hasa kipindi kama hiki cha masika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naomba sana Serikali iongeze bajeti ya Wizara hii hasa kwenye mfuko wa mazingira ili kuwezesha Wizara hii kutimiza majukumu yake muhimu sana kwa Taifa hili kwenye masuala muhimu yahusuyo mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.