Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuipongeza Wizara ya Katiba na Sheria na hasa Mahakama kwa kusimamia sheria na haki za Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kushauri Serikali, kama ilivyopendekezwa na Kamati ya Bajeti, kuhakikisha fedha zilizotengwa kwa maendeleo zipelekwe ili kukamilisha miradi ya maendeleo. Maeneo mengi yakiwemo miji na miji midogo haina Mahakama au miundombinu imechakaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji Mdogo wa Mbalizi hauna jengo la Mahakama badala yake shughuli za Mahakama zinafanyika kwenye jengo lililopo katika soko kwenye msongamano mkubwa. Napendekeza na kusisitiza Wizara iharakishe ujenzi wa Mahakama ya Mbalizi kwa usalama wa watumishi wa Mahakama na hata watuhumiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.