Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kwanza kuunga mkono hoja hii.Wilaya ya Nyang’hwale haina Mahakama ya Wilaya na jengo la Mahakama, wananchi wanafuata huduma hiyo Geita umbali wa kilomita 180 kwenda na kurudi. Kwa hiyo,ni gharama kubwa hadi kesi kuisha na wengine kushindwa kumudu gharama za kwenda mara kwa mara Mahakamani hadi kufutwa kwa kesi na kukosa haki zao. Je,ni lini Serikali itaanzisha Mahakama ya Wilaya ya Nyang’hwale? Je,ni lini Serikali itaanzisha ujenzi wa jengo la Mahakama Wilaya ya Nyang’hwale?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja.