Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kupoteza muda napenda kuongelea kuhusu taratibu za kisheria. Moja, wananchi wapewe elimu kuhusu sheria mbalimbali, mfano, anakamatwa mwizi aidha anapigwa au anachomwa moto hadi kufa kabisa. Wananchi wanajichukulia sheria mikononi mwao, wananchi waeleweshwe umuhimu wa kulitumia Jeshi la Polisi kwa tatizo lolote linalotokea ikiwa mitaani, maofisini au kwenye mikusanyiko yoyote ya watu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Jeshi la Polisi litoe mafunzo kwa Askari wake ambao wanamhukumu mtuhumiwa kabla hata kosa lililomtuhumu halijajulikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakama nyingi ni chakavu sana kiasi kwamba nyingine zinavuja au wakati mwingine mafaili yanakosa mahali pa kuhifadhiwa. Tunaiomba Serikali ikarabati mahakama ambazo zimechakaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wazee wa Baraza wengine ni wala rushwa sana wala hawashughulikii kuleta haki katika kesi zinazopelekwa kwao, Serikali iangalie kuwaweka wazee wenye weledi katika mahakama ili haki itendeke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, makosa ya jinai, kuna wanaoshtakiwa kwa makosa mbalimbali ya jinai, lakini baadhi walipelekwa mahakamani kesi imezungushwa kiasi mwisho wake mtuhumiwa anaachiwa huru. Serikali ione umuhimu wa kudhibiti wenye makosa ya jinai, wachukuliwe hatua zinazostahiki na kuwaachia huru wale wenye tuhuma ambazo ni za kubambikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.