Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti nampongeza Mheshimiwa Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Katiba na Sheria kwa kupata fursa ya kuiongoza Wizara hii ya learned friends. Aidha, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe Mheshimiwa Waziri ahakikishe Mfuko wa Mahakama kwa Mwaka 2019/ 2020 unatumika vilevile kujenga Mahakama ya Wilaya ya Namtumbo pamoja na Mahakama za Mwanzo ambazo wamechukua viwanja vya kujenga kwa muda mrefu na hawajaanza kujenga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Namtumbo wa maeneo waliyochukua na kuweka vibao vya kuonyesha kama maeneo ya Mahakama wanashangaa hakuna kinachoendelea. Maeneo hayo ni pamoja na Kijiji cha Mawa. Naomba sana Wizara itenge fedha za Mfuko wa Mahakama tunazozipitisha kuanza kujenga Mahakama ya Wilaya ya Namtumbo na ikiwezekana na ujenzi wa Mahakama za Mwanzo walizozipanga kuanza kujenga katika Wilaya ya Namtumbo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na naomba kuwasilisha.