Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Balozi Dkt. Mahiga, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri na kuweza kuwasilisha hotuba yake hapa Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo masuala ambayo naomba kupatiwa ufafanuzi, ambayo ni haya yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, sheria zilizopitwa na wakati; kumekuwa na malalmiko mengi kuhusiana na Sheria nyingi kupitwa na wakati na kusababisha wananchi kutotendewa haki. Je, kuna utaratibu au mkakati gani ili kuhakikisha kuwa zile sheria zilizopitwa na wakati, Miswada inaletwa Bungeni ili kuzifanyia marekebisho au kuhuishwa.

Pili, hukumu kuandikwa katika lugha ya Kiingereza; naomba kujua ni kwa nini Serikali haijaweza kuweka utaratibu wa hukumu kuandikwa kwa lugha ya Kiswahili na kutenda haki kwa mshtakiwa kukata rufaa? Kwa sababu nilipotembelea gereza kuu Mkoa wa Iringa changamoto mojawapo ya wafungwa ilikuwa wameshindwa kukata rufaa kutokana na kutoelewa lugha iliyoandikwa na hasa kama huna Mwanasheria wa kukusaidia. Je, Serikali haioni kama hawatendi haki kwa wasiojua lugha ya Kiingereza? Naomba kujua mkakati wa Serikali kuhusiana na hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda wa mashtaka; naomba kujua umri wa mashtaka kwa sababu ipo kesi ya waliokuwa wafanyakazi wa kilichokuwa Kiwanda cha Kukata Almasi (Tancut Diamond Iringa), kiwanda kilifungwa mwaka 1995 kwa kuingia mufilisi, hivyo wafanyakazi hawajalipwa na toka wakati huo walifungua kesi dhidi ya Serikali lakini matokeo yake mpaka leo bado wanaendelea kuhudhuria mahakamani. Naomba ufafanuzi juu ya suala hilo kwa sababu linachukua muda mrefu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali kwa kutoa tamko la kumaliza mashtaka yanayohusu wanawake na watoto ndani ya miezi sita. Kwa hili napongeza sana, sababu katika Mkoa wetu wa Iringa kumekuwa na kesi nyingi za ubakaji watoto ambao zimechukua muda mrefu sana kwisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.