Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri na Naibu Waziri wake kwa kazi nzuri wanazofanya, kwa kweli Waziri na Naibu wapo karibu sana na Wizara hii na wadau wote wa michezo na sanaa katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, Rais juzi alimzawadia Peter Tino shilingi milioni tano na hali ya wachezaji wetu wa zamani ambao wamecheza mpira miaka ya 1980 ni mbaya sana. Mheshimiwa Rais ameonesha njia, najua TFF inajitawala haiko chini ya Wizara, lakini Wizara ndio custodian wa michezo nchini.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwa Wizara, wawashauri TFF katika bajeti zao angalau wachezaji walioshiriki timu ya Taifa miaka ya 1980 ambao sidhani kama wamebaki hata 10 au 15, najua yupo Manara, Kitwana na Mbwana nafiriki bado yupo, wawapatie bima kuwasaidia wachezaji hawa kwa mateso wanayoyapata sasa hivi mitaani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumeona Jellah Mtagwa namna alivyotumikia Taifa katika michezo hasa mchezo wa mpira. Katika miaka ya 1990 na 1980 Jellah Mtagwa alitumika picha yake kwenye stempu za Tanzania; Shirika hili la Posta sasa hivi lina wajibu wa kumkumbuka Jellah na kumsaidia kwa mateso ya magonjwa ambayo anayo sasa hivi. Ushauri wangu TFF iwakatie bima wachezaji wote wa zamani ambao wako hai ili waepukane na mateso ya maradhi ambayo wanayapata. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile wachezaji wote waliocheza timu ya Taifa upo wajibu wa TFF kuweka majina yao kwenye uwanja mpya wa Taifa ili kuwa-inspire wachezaji wapya na wakumbukwe kwa picha na majina kwa namna walivyochangia ushindi. Wapo wachezaji waliocheza goal stage bado wapo ili na wao waonekane na vijana wetu wawe inspired na wachezaji wetu wa zamani.

Mheshimiwa Spika, lingine ni Bodi ya Ligi ya TFF; tumeona namna wanavyo-approve viwanja vibovu vichezewe ligi. Wachezaji wakicheza kwenye viwanja vibovu na ambavyo vingi vipo wanaumia sana. vilabu hivi vinapata gharama kubwa sana kutibu wachezaji ambao wanacheza na wanaumia kwenye viwanja vibovu vya premium league. Naomba bodi hii sasa ivifungie viwanja vyote kwa msimu ujao ili kila kiwanja kiboreshwe na kitengenezwe vizuri na wale ambao viwanja vyao havitafungiwa watafute viwanja mbadala kuepuka wachezaji kuumia na viwango vyao kunini.

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii tena kumshukuru Rais kwa namna alivyochangia AFCON U-17 alitoa bilioni moja, tumefungwa, lakini tusikate tamaa bado tunayo nafasi. Vijana hawa wapewe moyo; hamasa zilikuwa nyingi, lakini maandalizi yetu hayakuwa mazuri. Kwa hiyo, nichukue nafasi hii kumshukuru Waziri na naunga mkono hoja. (Makofi)