Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, Baraza la Sanaa Taifa – BASATA; lengo la Baraza hili ni kuboresha ubunifu pamoja na kuibua vipaji mbalimbali pamoja na utafutaji wa masoko yenye ubora kwa wasanii.

Mheshimiwa Spika, COSOTA na BASATA; hivi vyombo viwili vinavyofanya kazi pamoja, lakini kuna changamoto kubwa kupitia mlolongo mrefu wa usajili kwa wasanii kupata (stamp) za TRA ili kazi ya msanii iingie sokoni na ukizingatia mikoani ofisi hizi zinalega na katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri kuna kanda hazina ofisi za Baraza hili COSOTA na BASATA na hii inapelekea kwa wasanii wachanga kushindwa kufuata hatua hizi na uchumi wao mpaka afike Dar es Salaam ndipo apate usajili. Je, hawaoni kwa kushindwa kupeleka huduma kila mkoa ni kuwaumiza wasanii ambazo wako tayari kusajili kazi zao na huku milolongo hii ikiwagharimu? Ni lini watajenga ofisi zao kila mkoa ili kuondoa usumbufu huu?

Mheshimiwa Spika, dhana ya kufungia vyombo vya habari; Sekta ya Habari tulitegemea lengo lake ni kuhabarisha kuelimisha kukosoa na kuburudisha, lakini dhana hii inabadilika kila siku kwa kufungia vyombo vya habari ambavyo vimekuwa vikifungiwa na kufunguliwa gazeti la Mawio Mwanahalisi, Raia Mwema, na baadhi ya redio. Ni kwa nini wanatoka katika dhana ya ukosoaji na wanataka kusifiwa tu?

Je, lengo la Wizara hii ni kwa nini linajikita zaidi katika masuala ya siasa na kuacha kufungia kazi za wasanii, filamu ambazo kimsingi ziko mtaani na zinaharibu jamii. Wana mpango gani katika suala hili kuchunguza kazi zinazosambaa katika jamii video, audio na picha chafu kwenye mitandao hawaoni kwamba wameshindwa?

Mheshimiwa Spika, Cyber Crimes Act na Sheria ya Takwimu. Makosa ya kimtandao ambayo kwa ujumla yanaminya uhuru wa kupata habari na kusambaza hili ni tatizo na limepelekea jambo hili kutumika zaidi kisiasa. Sheria hizi zinaminya uhuru wa kujieleza na kukiuka haki za binadamu.

Mheshimiwa Spika, ajira; malalamiko ya wasanii ni mengi katika tasnia hii hususan katika maslahi yao. Sanaa ni ajira, hivyo, tunaishauri Serikali kusimamia maslahi yao na mafao yao ili kuhakikisha wachezaji wasanii wanapata haki zao.