Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue fursa hii kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai na kuniwezesha leo kushika kalamu na kutoa mchango wangu kwenye hoja iliyo mbele yetu. Pia nichukue fursa hii kuwapongeza Waheshimiwa Mawaziri wote wawili kwenye Wizara hii Dkt. Harison Mwakyembe, Mheshimiwa Naibu Waziri Juliana Shonza pamoja na watumishi wote wanaohudumu katika Wizara hii, wote kwa pamoja nawapongeza sana kwa kufanya kazi kwa weledi na ufanisi mkubwa.

Mheshimiwa Spika, Redio Tanzania, TBC FM hii ni redio ya Taifa lakini usikivu wake katika baadhi ya mikoa ni mbaya sana na mikoa au wilaya zingine hakuna kabisa. Jambo hili linafanya jamii kubwa kukosa habari muhimu zinazohusu Taifa letu. Mfano katika Wilaya ya Liwale Mkoa wa Lindi redio hii haipatikani kabisa. Nimeliuliza jambo mara nyingi bila majibu.

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na mchakato wa kutafuta vazi la Taifa. Je, mchakato huu umefikia wapi? Hata hivyo yako mavazi yanayovaliwa hapa nchini hasa na wanawake wakati wakiwa kwenye sherehe mbalimbali. Je, hakuna sheria inayokataza mavazi hayo? Hapa nazungumzia yale mavazi ya nusu uchi yanayoacha maungo wazi.

Mheshimiwa Spika, ziko nyimbo zinazoimbwa na wasanii nyimbo hizo, hufungiwa baada ya wimbo husika kutoka je, hakuna sheria inayokataza wimbo kabla ya kutoka kupitiwa kwanza maudhui yake, kwani kufungia wimbo ambao umeshatoka haisaidii sana kwani tayari huwa umeshaingia kwenye mitandao ya kijamii.

Mheshimiwa Spika, lugha ya Kiswahili ni moja ya tunu ya Taifa letu; kwa nini basi Wizara haina mpango mkakati wa kukikuza Kiswahili ambacho sasa kimeanza kuharibiwa na vyombo vyetu vya habari, viongozi wa kisiasa na wasanii mbalimbali kwa kuchanganya na lugha nyingine kama vile kiingereza (KISWKINGE) jambo hili linaharibu lugha yetu ya Kiswahili, lakini pia yako magazeti yanashindwa kuandika Kiswahili fasaha. Imefika sasa kuwa na Chuo cha kufundisha Kiswahili na kutungwa kwa sheria ya watumishi wote wa vyombo vya habari na wasanii kupitia kwenye Chuo hicho cha Kiswahili ili tunu ya Taifa iweze kuhifadhiwa. Pia Chuo cha Sanaa Bagamoyo kipewe fedha za kutosha na kujengewa uwezo na miundombinu wezeshi. Vilevile chuo hiki kipewe pia jukumu la kusomesha lugha ya kisiasa, sambamba na somo la kukuza uzalendo.