Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, nimeona ni vema nami nikachangia mchango wangu mdogo katika Wizara hii ambayo inasimamia utamaduni wetu, sanaa na michezo.

Mheshimiwa Spika, napenda kuipongeza Wizara hii kwa kazi nzuri inayofanywa na Waheshimiwa Mawaziri wakiongozwa na Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe na Naibu wake, Mheshimiwa Juliana Shoza, Katibu Mkuu na uongozi mzima wa Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, pamoja na sifa hizi nzuri kwa Wizara hii bado kuna changamoto ya usikivu wa TBC Taifa, hususani katika Jimbo langu la Itigi na hasa katika Mji wa Itigi. Itigi kuna redio ya Kanisa Katoliki (Redio Mwangaza) ambao wamefunga mtambo wao ambapo umezuia kabisa matangazo ya TBC Taifa. Je, ni lini sasa TBC itasikika Itigi?

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na majibu ya Serikali mara kwa mara kuwa katika bajeti ya nyuma yaani miaka iliyopita kuwa Serikali itafunga mtambo Itigi ili kuifanya TBC Taifa isikike. Naomba sasa katika bajeti hii Serikali kwa maana ya Wizara hii sasa ifunge mtambo Itigi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii kwa asilimia 100.