Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, michezo ya ngumi. Michezo hii ni muhimu sana kwa uchumi wa vijana wa Tanzania lakini kuna shida ya mapromota wengi wanatumia nafasi zao vibaya kwa kupeleka wachezaji nje ya nchi na kuingia mikataba mibovu. Hata hivyo, naishukuru Serikali kwa kuunda Kamati ya Ngumi ambayo kwa muda mfupi imeleta mafanikio kuonyesha mwanzo mzuri.

Mheshimiwa Spika, ulingo. Tunaomba Serikali inunue ulingo mwingine ili kuongeza upana wa matumizi ya ulingo kwani kwa sasa upo mmoja tu.

Mheshimiwa Spika, mabondia wa kike. Tunaomba Serikali isaidie mabondia wa kike katika kuwasimamia kupata haki zao za kikatiba.