Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri, Olympic ni maarufu sana duniani kwa sasa. Ni michezo inayoendeshwa kwa ukwasi mkubwa wa fedha na hivyo Mataifa yanayoandaa yamekuwa yakijizolea mamilioni na mabilioni ya fedha za kigeni. Kwa nini Serikali haifikirii kujenga kituo cha michezo ya Olympic (Olympic Centre) katika moja ya fukwe zetu tulizojaliwa na Mungu kama vile ufukwe wa Kijiweni uliopo Mchinga Lindi?

Mheshimiwa Spika, Serikali ioneshe nia hiyo kwanza, kisha itafute wachezaji ambao wataingia ubia na Serikali katika kufanikisha jambo hilo muhimu kwa uchumi na maendeleo ya Sekta ya michezo nchini.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ni TBC kugeuzwa kuwa chombo cha chama badala ya kuwa chombo cha habari cha Taifa. Imefahamika kuwa duniani kote Television ya Taifa inafanya kazi kwa karibu na Serikali iliyopo madarakani, lakini TBC inavuka mipaka na hivyo kuondoa kabisa ladha ya kuendelea kuitazama na hamu ya kuipenda. Jambo hili halina afya njema kwa mustakabali wa Taifa linalokusudia kupiga hatua ya maendeleo na kufikia uchumi wa kati. Ujumbe wangu, TBC iache kushabikia siasa za mrengo mmoja pekee, inapoteza watazamaji na wasikilizaji wake kila kukicha.

Mheshimiwa Spika, jambo la tatu ni wazo la Serikali kuandaa mashindano maalum ya Insha yanayohusu Lugha ya Kiswahili ili kuongeza hamasa na hulka ya vijana wetu kuipenda, kuithamini na kuienzi lugha yetu hii. Mheshimiwa Waziri, mashindano haya yanaweza kuanzia ngazi za Shule za Msingi hadi Chuo Kikuu. Ahsante.