Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kumekuwa na mafanikio yasiyo endelevu kwenye Sekta ya Michezo, hii ni kwa sababu wanamichezo wetu wanakosa misingi imara ya kitaaluma kimichezo. Msingi wa kitaaluma unaweza kupatikana vizuri zaidi kupitia shule zetu kwa ngazi mbalimbali kuanzia Shule za Chekechea na kuendelea. Kikwazo kikubwa kimekuwa ni kutokuwa na Walimu ambao ni Wataalam wa Michezo na Miundombinu ya kutumia kushiriki michezo, hali ambayo imekuwa inaathiri sana vipaji vya wanamichezo.

Mheshimiwa Spika, hivyo nashauri, michezo iwe ni moja ya masomo katika mitaala ya shule zetu hali ambayo itafanya watoto wote wenye vipaji mbalimbali waweze kuviendeleza. Kuwe na mkakati maalum wa kuandaa walimu watakaotumika kuwafunza vijana wetu na kukuza vipaji mbalimbali kwenye shule, vilabu vya michezo na kadhalika. Kwa mfano, timu zetu za mpira wa miguu hivi sasa zinafundishwa na walimu kutoka nje na hakuna idadi kubwa ya walimu wa Kitanzania wanaofundisha soka nje ya nchi.