Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii muhimu. Awali ya yote nimshukuru kwanza Mwenyezi Mungu ambaye amenipa afya na nguvu kuendelea kuwatumikia wananchi wangu wa Jimbo la Kyerwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri anazozifanya. Kwa kweli nampongeza sana, tumeona mabadiliko makubwa ambayo amekuwa akiyafanya, kwa kweli tunampongeza pamoja na wasaidizi wake, wanafanya kazi nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia mimi nilipongeze Jeshi letu la Polisi, kwa kweli pamoja na baadhi ya wenzetu kubeza na kusema hakuna chochote kinachofanyika na wengine wamefika mbali kusema maneno magumu, wanasema Jeshi la Polisi ni kansa, kitu ambacho kwa kweli si jambo zuri na sikutegemea kama Mbunge angeweza kusimama na kusema neno la namna hii. Tuko hapa kwa sababu ya kazi nzuri zinazofanywa na Jeshi letu la Polisi. Ndugu zangu tunaweza tukawa hatuelewi lakini ukiongea na majirani zetu ambao wanapita kwenye nyakati ngumu, ndiyo mnaweza mkajua umuhimu wa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa kazi nzuri wanazozifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunalala wenzetu wako nje wanang’atwa na mbu na mambo mengine wanayoyafanya. Leo hii tuko hapa tumetulia, hali ni nzuri, ukienda nchi za wenzetu, tulienda kule Burundi, kila mnapozunguka mnatembea na mitutu ya bunduki lakini nendeni pale nje hata bunduki hatuzioni ni kwa sababu ya amani iliyopo katika Taifa letu.

MHE. JOHN W. HECHE:Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utaratibu.

MWENYEKITI: Mheshimiwa, kuhusu utaratibu, nisaidie Kanuni.

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kanuni ya 64(1)(a), Mbunge hatatoa Bungeni maneno yasiyokuwa na ukweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa Bungeni tuko hapa kwa ajili ya….

MWENYEKITI: Maneno ambayo siyo ya ukweli ni uongo, si ndiyo?

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo uwongo huo. Hakuna miongoni mwetu hapa ambaye anabeza kazi ya Jeshi la Polisi.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, anachojitungia na kutaka kujipa uhalali kwamba Jeshi la Polisi sisi tunalibeza, hatulitaki au…

MWENYEKITI: Mheshimiwanimekuelewa, sababu ya muda, nimekuelewa, kaa tu, sitaki usimame. Anachosema Mheshimiwa Bilakwate, nimemsikia vizuri sana halafu asubuhi nilimsamehe sana huyu Mheshimiwa Sophia Mwakagenda alitumia neno, Jeshi la Polisi ni kansa, nilimvumilia.Sasa Mheshimiwa Bilakwate anajibu kwa namna hiyo, ndiyo maana sitaki mimi niliendeleze suala hili. (Makofi)

Mheshimiwa Bilakwate,hoja yako imesikika lakini nalikataza hilo, sitaki kufika huko.

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Niombe sanaWizara ya Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Waziri lakini Mheshimiwa Waziri wa Fedha, Jeshi letu la Polisi kwa kazi nzuri wanazozifanya waweze kupewa yale ambayo ni mahitaji yao lakini bajeti yao izingatiwe ili waweze kuendelea kutimiza majukumu yao. Vinginevyo tusipowajali hawa wenzetu wanaosema wao wako wengi siku wakianzisha vita, tusipowapa vitendea kazi vizuri ili waweze kuwadhibiti watakapoanzisha vita, tutakuwa tunakwenda pabaya. Kwa hiyo, niombe sana tuwasaidie Polisi wetu kwani wanayo mahitaji mengi ili waweze kutimiza majukumu yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, Mheshimiwa Waziri ulifika Kerwa, ulionamazingira ambayo Polisi wetu wanafanya kazi. Uliona Kituo chaPolisi siyo kizuri na kituo kile ni ofisi za kata, nikuombe sana hili ulizingatie. Sisi tuko mpakani, tunakutana na watu wengi, majirani zetu wanaingia, tusipoimarisha vizuri Jeshi la Polisi mipakani, tunaweza tukaingiza mambo mengine ambayo baadaye yanaweza kuhatarisha amani ya taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine ni kwa upande wa NIDA. Kerwa tupo kwenye utaratibu wa kuanza kusajili vitambulisho vya NIDA, nikuombe sana Mheshimiwa Waziri, hii mikoa ambayo iko pembezoni muweze kuiangalia kwa umakini sana kwa sababu wako wenzetu wanatamani kuwa Watanzania ambao hawana sifa. Suala hili tuliangalie ilitusijetukaingiza watu ambao hawana sifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mwingine tunahitaji hata kuhubiriana injili au kukemeana mapepo. Naomba nisome hili nenona mwenye akili ataelewa. Nasoma Kitabu cha Warumi 13:1-7, inasema: “Kila mtu naaitii mamlaka iliyo kuu;kwa maanahakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo imeamuriwa na Mungu. Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana naagizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu. Kwa maana watawalao hawatishi watu kwa sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka?Fanya mema, naweutapata sifa kwake. Kwa kuwa yeye nimtumishi wa Mungu kwako kwa ajili ya mema. Lakini ufanyapo mabaya, ogopa; kwa maana hauchukui upanga bure; kwa sababu ni mtumishi wa Mungu, amlipiziaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu. Kwa hiyo ni lazima kutii, si kwa sababu ya ile gadhabu tu, ila na kwa sababu ya dhamiri.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kuhusu Utaratibu.

MWENYEKITI: Kanuni gani?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kanuni ya 64(1)(a), inasema: “...hatatoa ndani ya Bunge taarifa ambazo hazina ukweli”.

MWENYEKITI:Hicho ni Kitabu Kitakatifu, Mheshimiwa endelea.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sijasema sababu.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.Niendelee kusoma mstari, nilikuwa nimefika mstari wa6 unasema: “Kwa sababu hiyo tena mwalipa kodi; kwa kuwa wao ni wahudumu wa Mungu, wakidumu katika kazi iyo hiyo. Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru;astahiliye hofu, hofu; asitahiliye heshima, heshima”.Haleluya.(Makofi)

WABUNGE FULANI: Ameen.

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema haya nafikiri kila mtu ameelewa, kama mnataka Jeshi la Polisi lisiwapige na lisizuie mikutano lazima muwe watii.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA:Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Nyie mnasema mnaonewa kila sehemu, mnaonewa wapi nikwa sababu hamtendi mema. Mabaya mnayoyatenda ndiyo yanayowageuka, tendeni mema muone kama na ninyi hamtatendewa mema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nakushukuru.(Makofi)