Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba nianze kwa kuipongeza Wizara ya Elimu kwa kazi nzuri wanazozifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, binafsi naona juhudi za Mheshimiwa Waziri pamoja na wasaidizi wake, kwa kuendelea kuongoza vizuri Wizara ya Elimu. Nianze kwa kuishukuru Serikali kwa kuendelea kuboresha mazingira ya kufanyia kazi Wakaguzi wa shule, yaani wadhibiti elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kuamua kuwajengea Ofisi katika Wilaya 100 ambazo zitawasaidia kuwa na mazingira mazuri ya kufanyia kazi. Nashukuru katika Wilaya 50 zinazoanza, Wilaya ya Meatu imo na tayari Wilaya hizo 50 zimeanza kuletewa fedha za kujengea Ofisi zao. Naamini muda wowote pia Wilaya ya Meatu nayo itaingiziwa fedha tayari kwa kuanza kujenga Ofisi ya Wadhibiti ubora wa elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa hatua ya makusudi iliyochukua kuweza kunusuru maboma yaliyokuwa yameanzishwa na wananchi ili nguvu za wananchi zisipotee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali kwa makusudi ya hatua ilichukuwa ya kuweza kunusuru maboma yaliyokuwa yameanzishwa na wananchi ili nguvu za wananchi zisipotee, binafsi nishukuru kwa Mkoa wa Simiyu tumeletewa Sh.1,337,500,000 kwa ajili ya kukamilisha madarasa ya sekondari 107. Naishukuru sana Serikali kwa hiyo nguvu za wananchi hazitapotea bure. Hata hivyo, binafsi nikupongeze wewe binafsi huwezi kujisemea kwa kazi nzuri unazozifanya Jimboni kwako kwa fedha zako binafsi kwa kuanzisha maboma na hatimaye leo umepewa maboma 54 yakiwa kwa Halmashauri ya Bariadi DC na Bariadi TC hiyo ni juhudi yako ndiyo maana umeletewa mengi. (Makofi)

Pamoja na hayo Serikali inatoa fedha nyingi sana kwa ajili ya elimu ikiwepo elimu bila malipo. Kwa makusudi Serikali imeamua kuifanya elimu ya sekondari kuwa elimu ya lazima. Pamoja na fedha nyingi zinazotolewa na zinatumika kama zilivyokusudiwa nilikuwa nina wazo moja la kuweza kuboresha ili fedha zitumike kama zilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo changamoto kubwa katika sheria. Sheria ya kuhakikisha mwanafunzi akianza sekondari ya kumbakisha mpaka anamaliza, zipo sheria ambazo zinasema mtoto haruhusiwi kupata ujauzito au kuoa au kuolewa lakini sheria ya kumbakiza shuleni haipo. Naomba Wizara ione iweze kuleta sheria ili tuweze kuipitisha ili Walimu wasiwe na matatizo, wale wanafunzi wanaokatisha masomo waweze kuchukuliwa hatua na hatimaye warejee mashuleni.

Mheshimiwa mwenyekiti, lakini Mkoa wetu wa Simiyu unayo changamoto kubwa tatizo la mimba kwa wanafunzi bado ni kubwa kwa mwaka 2017 tulikuwa tunamimba 196, mwaka 2018 mimba 187 lakini kwa makusudi wananchi wameanza kujenga hosteli kwa ajili ya watoto wa kike. Ombi langu kwa Serikali ni ku-support nguvu za wananchi ili mabweni yale yaweze kukamilika na yanufaishe watoto wao. Manufaa si tu kwa ajili ya kupunguza mimba za wanafunzi, bali pia itawaweka pamoja wanafunzi wawe na mawazo pamoja wawapo shuleni na kuondokana na mawazo ya mtaani, lakini pia itaongeza ufaulu hususan kwa watoto wa kike kwa kuwa maeneo yetu yanafahamika hamna maeneo ya kuishi inabidi wakae kwenye majumba ya ndugu na jamaa na unavyojua tabia zetu sisi ukikaa mahali lazima ufanye kazi huwezi kukaa tu kwa ajili ya kusoma, lazima ufanye kazi katika familia unayokaa lakini hii pia inapunguza pia kiwango cha ufaulu kwa watoto wa kike. Pia mabweni haya yatapunguza ule utoro kwa wanafunzi, wanafunzi wamekuwa wakiacha masomo kwa sababu ya kutembea umbali mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jamii yetu pia ni wafugaji, kwa hiyo kuwepo na mabweni kutawasaidia wanafunzi wale wabaki mashuleni. Binafsi niipongeze Wilaya ya Meatu kwa juhudi zake binafsi kwa kuanzisha shule maalum ya makao kwa ajili ya watoto wa wafugaji ili waweze kubakia pale. Niiombe Serikali iweze kuwasaidia juhudi waliyofikia. Wamekamilisha madarasa manne, wamejenga maabara mawili yanahitaji kukamilishwa, wamejenga bwalo moja linatakiwa kukamilisha. Namwomba Waziri mgawo utakaopatikana waione pia Shule ya Sekondari Makao ambayo iko katika Kata ya Mwangudo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, toka nianze Ubunge wangu hapa niliikuta shule ya High School ya Nyalanja ina madarasa sita ambayo hayafanyi kazi kwa kuwa hawana bweni. Shule ile ni ya bweni upande wa High School na O-level ni shule ya kutwa. Naomba basi ili kuwepo na thamani ya fedha yale madarasa sita yapatiwe bweni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekuwa mara nyingi namfuata Waziri pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, naomba basi katika bajeti hii waisaidie High School ya Nyalanja ipate bweni tuweze kupata mchepuo mwingine ambao pia utawaleta watoto wa kutoka mikoa mingine. Sambamba na hilo pia inawasaidia wanafunzi wa shule ya kutwa wa O-level kuweza na wenyewe kuvutiwa kupata matamanio na wenyewe waweze kufika kama wenzao walivyofikia.

Mheshimiwa mwenyekiti, lakini niseme changamoto moja ambayo niliiona wakati wa ziara tukikagua LAAC, ni gharama kubwa ya kuweka umeme katika shule. Shule inaomba kuwekewa umeme inapohitaji kuweka transformer TANESCO inaiagiza shule ilipie, wakati huo shule haina uwezo wa kulipia gharama hizo kubwa kama milioni 12. Naamini kwamba transformer ile ikienda itasaidia pia kijiji kwa sababu katika yale maeneo kuna taasisi nyingine za Serikali pamoja na kijiji kwa hiyo haitafanya kazi tu kwa ajili ya Sekondari. Niiombe sasa Serikali itoe zile fedha zenyewe badala ya kuiagiza shule itoe zile fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hayo machache, naomba kuunga mkono hoja na nakushukuru sana. (Makofi)