Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia fursa hii, ya mimi nami kuweza kutoa mchango wangu, katika Wizara hii ya Elimu, naomba ku-declare interest ni mdau wa shule binafsi na mwalimu kwa taaluma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuweka tu rekodi vizuri, kwa mchango wa Kaka yangu Kigola, ninaomba ndugu zangu Watanzania, tutofautishe English Medium Schools na International Schools hivi ni vitu viwili tofauti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, English Medium Schools ni hizi ambazo hakuna English Medium School Tanzania ninayoifahamu ambayo ina-charge zaidi ya 4.5 milion, hakuna hata moja, hata moja, zingine zote zinazo-charge above that ni International Schools. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu mjadala tulishaufunga ni uchaguzi huria, kama ilivyo hoteli kama ilivyo huduma nyingine yoyote, nadhani ifike mwisho mambo ya kujadili ada elekezi na vitu vya namna hiyo kwa sababu mtu halazimishwi.

MBUNGE FULANI: Tuongelee humu ndani.

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, amlete shuleni kwangu ada ya day ni laki nane na nusu kwa mwaka, milioni mbili kwa mwaka kwa bweni, mwambie aje kwangu, hiyo nayo itamshinda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuweka hiyo rekodi sawa, ninaomba sasa nimpongeze sana Mheshimiwa Prof. Ndalichako, kwa kazi nzuri inayofanyika ya kuinua Elimu katika nchi hii. Naibu wako Mheshimiwa Ole Nasha, Dkt. Akwilapo, Katibu Mkuu, Mama Ave Maria Naibu Katibu kwa kweli watu hawa wanaipeleka elimu yetu mahali pazuri pamoja na kwamba changamoto ndogo ndogo zipo nina hakika nia ya dhati na njema ipo ya kuhakikisha tunamaliza changamoto hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizo ninaomba kwa vile mengi yatasemwa na wenzangu, nijikite kwa yale ambayo sisi tulioko kwenye field ndiyo tunayapitia na hakuna mwingine wa kuyasema isipokuwa sisi tulioko huko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba hili lisichukuliwe kwamba tumekuja humu ndani kwa sababu ya maslahi binafsi, ninaweza kufa kesho na kesho kutwa, lakini Watanzania wapo, vizazi vyetu vitabaki, tunachotaka ni kuboresha elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Elimu, ni uwekezaji, tunazungumzia Uwekezaji wa vitu vingi, Rais amekuwa akipigania kuhakikisha wawekezaji wanakuja kuwekeza Tanzania ili kuweza kupata fedha za Kigeni, na hatimaye Watanzania wapate ajira na vitu vya namna hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naomba nimuombe Rais, aangalie suala zima la Uwekezaji kwenye Elimu. Tunaweza tukawekeza kwenye Viwanda, ikiwa hatujawa- train watu wetu vizuri, inavyotakiwa bado uwekezaji wetu katika maeneo mengine unaweza usiwe wa tija sana. Nikizungumza hili ninajua Mheshimiwa Dada yangu Angellah Kairuki, sasa umepewa nafasi ya uwekezaji, kusimamia uwekezaji katika nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakuomba sana tuwekee dirisha la wawekezaji wa Elimu Tanzania, maana hawa ndiyo wanaowajenga wataalamu wetu watakao iendesha nchi hii kesho na kesho kutwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikisema hivi ni kwa sababu ya gharama kubwa ya uendeshaji wa shule hizi, ujenzi wake na vitu vya namna hiyo. Niliwahi kusema Uganda, ukifahamika tu wewe unataka kujenga shule, wanakuondolea VAT kwenye constructions material zote, zote unaondolewa, kwa sababu wanajua unakwenda kuwekeza kwa ajili ya jamii ya kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo na sisi tuangalie, namna ambavyo tutaweza kupunguza gharama zingine kwa wamiliki na waendeshaji wa hizi shule, tunapitia wakati mgumu sana. Niliwahi kusema ukiwapima waendeshaji wa shule, wengi wana pressure na sukari kwa sababu ya changamoto ya uendeshaji wa hizi shule. Nikisema hivi changamoto, mojawapo kwa mfano, vitabu, suala la vitabu, mwaka juzi tulizungumza hapa na vile vitabu vikaondolewa kwenye system.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jukumu la vitabu kutunga, kuvihakiki, kuvisambaza na kazi zingine zote imepewa TET au TAI lakini kwa bahati mbaya tu naomba Bunge lako Tukufu lifahamu ya kwamba TET hawajawahi kututungia vitabu watu wa English Medium schools mpaka leo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa pata picha hawa watoto wanafundishwaje na ni watanzania na wako kwa mujibu wa Sheria? Ninapozungumza hivi ni pamoja na kutokuwa na mtaala wa lugha ya kiingereza, pamoja na kutokuwa na vitabu, hii inaleta mno changamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia jambo lingine ni TET hawa hawa wamepewa I mean, mandate ya kuhakikisha wanatoa ithibati kwa waandishi wa vitabu vya ziada, jambo ambalo mpaka sasa, kuanzia 2015 hakuna mwandishi wa vitabu vya ziada aliyepewa ithibati na TET na watu wa English Medium wamekuwa wakitumia vitabu hivyo hivyo vya waandishi vya ziada visivyo na ithibati ndivyo vinavyotumika kufundishia, pamoja na kwamba bado hizo shule zinajitahidi kujikongoja kufanya vizuri katika mitihani hii ya mwisho ya kitaifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwaombe sana Mheshimiwa Prof. Ndalichako, naomba ufatilie suala TET, TET wanakuangusha, wao ndi wenye mujibu wa kutoa hivyo vitabu na mihutsari na mitaala. Tunaomba basi waangalie na hawa watu wa English Medium kwa jicho la huruma. Kama vile haitoshi, walimu wa shule za Serikali wamepatiwa mafunzo ya jinsi ya kutumia huo mtaala mpya wa Kiswahili uliotoka, lakini kwa bahati mbaya sana, walimu wanaofundisha private schools hawajapewa mafunzo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na juzi, wametoa barua TET ya kwamba ukitaka ku-train mwalimu kupata elimu ya huu mtaala mpya kila mwalimu anatakiwa alipiwe shilingi laki tatu. Hawa walimu wanawafundisha wa-Nigeria au ni watanzania? Kuna vitu vingine sijui kama hata Rais anavifahamu ama Wizara inavijua kwa style hiyo. Hebu pata picha tuna walimu zaidi ya 40,000 wa private schools, 40,000 mara 300,000 ni over 12 Bilioni wanazifanyia nini? Hizi pesa? Wakati TET iko pale, kwa ajili ya kutoa na kusimamia Elimu mitaala na miongozo, hii haiko sahihi tunaomba watuangalie na sisi ni watanzania, tunafundisha watoto wa Kitanzania, ndiyo wako humu wengine wamesoma wakina Mlinga hawa wamesoma English Medium leo ni Wabunge wazuri kama mnavyo waona wasingesoma huko, wasingekuwa hivyo kwa hiyo TET tunaomba watuangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kingine kwa haraka mwaka juzi Waziri alifuta kodi ya zimamoto humu ndani, nilipongeze hilo Jeshi letu, linafanya kazi vizuri, wamekuja hapa juzi wametupa Elimu ya namna ya kuzima moto sisi Waheshimiwa Wabunge. Lakini cha kusikitisha kodi hiyo imerudishwa kwa mlango wa nyuma, ukaguzi wa masuala ya zima moto unalipia Certificate shule, laki 500,000 lakini ile elimu ya kuja kupambana na habari ya kuzima moto, kila mwanafunzi anachajiwa shilingi 20,000 ina maana shule ikiwa na wanafunzi 500 unalipa shule yako milioni 10, kwa nini inaonekana kama vile kwenye private schools ndiyo mahali pekee pa kuchukulia pesa? Kwa nini, kwa nini?

Mheshishimiwa Mwenyekiti, juzi sisi Wabunge tumefundishwa hapa, ni ile ya kuweka tu petroli pale na kuzima ule moto, wanafunzi wa private wanatakiwa walipe 20,000 kila kichwa, tunakoelekea ni wapi? Yaani private schools zimekuwa ni vyanzo vya kutafutia pesa kweli? This is not fair? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna swali liliulizwa juu ya watoto yatima hapa na watoto wa mitaani, na vitu vya namna hiyo, naomba nitoe mapendekezo kwa Serikali yangu, tunafundisha watoto, nimemsikia hata mwenzangu, Mheshimiwa Shangazi akizungumza hizi shule za Makanisa, ndiyo zinasaidia yatima, on board shuleni kwangu nenda leo wako 50 over 200 wamemaliza shule watoto yatima waliokuwa mtaani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, on board wako 50, lakini bado pesa kama hizi unatakiwa uzitoe kweli, mngetuacha tuwasomeshee watoto hawa mtaani, kupunguza haya majanga? Na watu wa private pia wameomba ikiwezekana hata wapangiwe idadi kadhaa ya wale watoto kila mkoa, kulingana na shule zilizoko, wachukue wale watoto yatima na watoto mtaani, wawasomeshe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, waachwe kufatwa fatwa na hivi vitu vingine kama mara kodi fire, mara rent, sijui land rent na vitu vingine visivyo na tija. Kwa hiyo, nilifikiri private schools ni mahali peke yake ambako watoto hawa wa mtaani wanaweza kuwa absorb na wakasaidiwa na tukamaliza janga la watoto wa mtaani katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba tunapata dialogue nzuri sasa hivi, nimpongeze sana Mheshimiwa Prof Ndalichako, pamoja na Katibu Mkuu at least wanatushirikisha kwenye baadhi ya mambo mengi sasa kuhakikisha kwamba kunakuwa na fair play katika uendeshaji wa hizi shule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema mambo haya ya msingi kabisa, hasa suala la vitabu tunaomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja atuambie ni lini TET watatoa vitabu kwa ajili ya hizi shule za kiingereza na lini hasa tutapata mitaala na lini hasa na ni kwa nini wanachaji shilingi 300,000 kwa kila mwalimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukipeleka huyo mwalimu kwenye hiyo kozi kumbuka unamlipia gharama za usafiri, chakula, malazi, ina maana mwalimu mmoja ana-cost shule zaidi ya shilingi milioni moja, haya kuna shule zina walimu mpaka 400, 450 huyo mwenye shule anazipata wapi hizo pesa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutamkamua huyo mzazi anayesomesha watoto wake kwenye hizi shule mpaka lini? Naomba kuunga hoja mkono lakini mama Ndalichako, ukija hapa tunaoamba utuletee majibu ya haya. (Makofi)