Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, awali ya yote kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa nafasi tena ya kuweza kurudi ndani ya Bunge hili Tukufu. Lakini vilevile niwashukuru wapiga kura wangu akina mama wa Mkoa wa Njombe kwa kuniamini na kunichagua kuwa mwakilishi wao, ahsanteni sana akina mama. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumpongeza, Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwa taa ya ulimwengu. Hivi sasa Mataifa mbalimbali yamekuwa yakimzungumzia kwa utendaji wake wa kazi mzuri. Gazeti la New York Times nchini Marekani limemzungumzia na kumwelezea vizuri katika suala zima la uadilifu na utekelezaji wa sera aliokuwanao tangu alipokuwa Waziri kwa kipindi cha miaka 20. Pongezi sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna gazeti lingine nchini Uingereza linaitwa London Times, limeelezea jinsi wananchi wanavyomshauri Malkia Elizabeth kuwa siku ya yake ya kuzaliwa iwe siku ya usafi nchini Uingereza. Hii yote ni kwa sababu ya utendaji mzuri wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, ndiyo maana watu sasa hivi wanatamani ku-copy mambo yake. Hongera sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala la elimu. Naanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuweza kutukeleza ahadi yake katika suala zima la elimu, kwa maana ya kwamba ada kuanzia shule ya msingi hadi kidato cha nne imefutwa. Ni kweli sasa hivi wanafunzi wa shule ya msingi hadi kidato cha nne hawalipi ada tena. Vilevile ahadi yake ya kutoa vitabu kuanzia shule ya msingi mpaka kidato cha nne pia imetekelezeka. Hongera sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuishauri Serikali na kuijulisha kwamba dhana hii ya kufutwa kwa ada bado haijaeleweka kwa wananchi. Hivyo basi, naishauri Serikali ishuke chini kwa wananchi ili iwaeleweshe vizuri dhana nzima ya elimu bure, kwa maana ya ufutwaji wa ada kutokea shule ya msingi mpaka kidato cha nne, lakini vilevile na Serikali kuchangia vitabu kuanzia shule ya msingi mpaka kidato cha nne.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala la huduma ya afya. Nitakuwa mchoyo wa fadhila nisipoendelea kumpongeza Mheshimiwa Rais wangu kwa sababu hivi sasa tumeona ameweza kutatua kero mbalimbali katika Wizara ya Afya kwa muda mfupi sana aliokuwa madarakani. Kero kubwa ya CT-Scan katika hospitali ya Muhimbili imetekelezeka. Wananchi wanapata kipimo hiki cha CT-Scan ndani ya Hospitali ya Muhimbili ukilinganisha na zamani walikuwa wanaenda kupima kipimo hiki nje ya hospitali kwa gharama kubwa. Hongera sana Mheshimiwa Rais.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tumeona uanzishwaji wa maduka ya madawa ya MSD ndani ya hospitali ya Muhimbili na kule Mwanza. Hivi sasa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam ambao wanakwenda kupata matibabu pale Muhimbili na wananchi wa Jiji la Mwanza wanapata dawa kwa bei nafuu. Hongera sana Mheshimiwa Rais kwa kutekeleza hilo ndani ya muda mfupi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeanza kuona mabadiliko ya wafanyakazi katika hospitali, lakini vilevile na vituo vya afya. Hii inapelekea zile ziara za kushtukiza katika hospitali hizi na vituo vya afya.
Rai yangu kwa Serikali, naomba sasa Serikali ishuke, iende kwenye mikoa mingine ili iweze kutatua kero ambazo zinawakabili wananchi wa mikoa mingine katika hospitali. Mfano kule kwetu Njombe, hospitali yetu ya Njombe sasa hivi imekuwa ni chakavu sana; haina dawa za kutosha, haina wahudumu wa kutosha wala hospitali hii haina vipimo, ukizingatia kwamba hospitali hii ya Njombe sasa hivi tunaitegemea kama hospitali ya Mkoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Halmashauri ya Njombe Mji wanatibiwa pale, wananchi wa Halmashauri ya Wanging‟ombe wote wanatibiwa pale. Namwomba Waziri, Dada yangu Mheshimiwa Ummy Mwalimu, tukitoka kwenye Bunge hapa mje kuona jinsi ilivyochakaa, dawa hakuna, hatuna Madaktari wa kutosha na vipimo hakuna. Nawaomba mje kuangalia changamoto hii ili muweze kututatulia, kwa sababu sisi mkoa wetu wa Njombe ni mkoa mpya, tunahitaji kupata, hospitali ya uhakika.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile napenda kumwomba Mheshimiwa Simbachawene kwamba katika mkoa wetu wa Njombe, tuna Wilaya mpya ya Wanging‟ombe, Wilaya hii haina hospitali ya Serikali. Wananchi wa Wanging‟ombe…
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.