Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa pongezi kwa kazi nzuri zinazofanywa na Serikali kupitia Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaunga mkono hotuba endapo nitapata jibu sahihi na nitashika shilingi ya mshahara endapo sitapata majibu sahihi ya kujengewa Chuo cha VETA Kwimba ambapo ni ahadi ya Serikali. Waziri na watendaji ni waungwana sana lakini cha kushangaza kwa zaidi ya miaka 15 kumekuwa na ahadi ndani ya Bunge na kwenye vitabu lakini utekelezaji ni zero. Mimi ni Seneta humu Bungeni siyo vizuri sana kukaa naulizia suala hilo hilo kila Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kwimba ilikuwa moja ya wilaya iliyokuwa imepangiwa kujengewa Chuo cha Ufundi miaka 10 iliyopita. Wilaya ya Kwimba kutokana na agizo la Wizara tuliambiwa tutafute eneo ambapo tayari eneo lipo la ekari 60 na lina hati ya umiliki chini ya Halmashauri ya Kwimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua kutoka kwa Mkurugenzi wa VETA, ni nani aliyefuta Wilaya ya Kwimba kwenye orodha ya wilaya zilizopitishwa kujengewa chuo cha VETA? Mkurugenzi wa VETA, Dkt. Pancras Bujulu, naomba kupitia Wizara ya Elimu nipate ahadi, dhamira, kukiri, kutimiza ahadi (commitment) ya kujengewa Chuo cha VETA ambapo ni ahadi ya Serikali kwa zaidi ya miaka 10.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri arejee andiko langu hapo juu kuwa sitaunga mkono na nitashika shilingi endapo sitapata commitment ya Serikali. Mheshimiwa Prof. Joyce Ndalichako namheshimu sana, naomba yeye na viongozi wenzake hiki kilio cha VETA kifikie ukingoni.