Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Mansoor Shanif Jamal

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. MANSOOR S. HIRAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru umenipa nafasi na mimi nichangie hoja iliyo mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema niweze kusimama mbele yako kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Kwimba kuzungumza kuhusiana na suala la maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala la maji naomba niseme mambo matatu. La kwanza, kuna Mradi wa Shirima; ulianza mwaka 2013, mwaka jana ulipofanya ziara kwenye Jimbo la Kwimba nilienda na wewe tulikupeleka mpaka kwenye mradi huo wa Shirima, Kata ya kukibizi, ulitoa ahadi kwamba mradi ule utakamilika ndani ya miezi mitatu. Mheshimiwa Waziri mradi bado haujakamilika, nashukuru mkandarasi huyo mkataba wake ulikuwa ume-expire, tarehe 28.03.2019 Serikali imekataa ku-extend mkataba huo na imekabidhi ule mradi kwa MWAUWASA ili waweze kuumalizia. Naomba Mheshimiwa Waziri uwaambie MWAUWASA waumalize mradi huo mapema sana kwa sababu wananchi wana shida sana ya maji kwenye Kata hii ya Kikubizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo napenda kulizungumzia ni kwamba kuna maombi ya mradi wa tenki la kutunza maji Ngudu. Wilaya ya Ngudu ni Makao Makuu ya Wilaya ya Kwimba lakini tuna matatizo ya maji, wakati KASHWASA wanapofanya matengenezo kwenye tenki ya Mhalo wananchi wa Ngudu wanakosa maji. Tumepeleka maombi Wizara ya Maji kupata tenki ya lita milioni tatu. Mheshimiwa Waziri maombi yako kwenye Wizara yako naomba utusaidie ili wananchi waweze kupata maji ya uhakika Wilayani Kwimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine kuna mradi wa tenki ya Kizida. Tunaomba pesa kutoka Mfuko wa PBR na maombi yameenda siku nyingi yako Wizarani yanasubiri majibu. Tunaomba mradi huo ukamilike kwa sababu ukikamilika Vijiji vya Shikangama, Shilembo, Nguliku, Mwamakelemo, Ilula, Kibitilwa, Mwamapalala vyote vitapata maji. Naomba Mheshimiwa Waziri usikie kilio chetu cha maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kwamba Wilaya ya Kwimba ni Wilaya ambayo tabianchi imetuathiri sana, hatuna ziwa wala mito ambayo ina maji ya kudumu tunatemegea visima…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. MANSOOR S. HIRAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, naunga mkono hoja. (Makofi)