Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nianze kwa kuunga mkono hoja. Naungana na Waheshimiwa Wabunge wenzangu ambao walipata fursa ya kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na timu yote kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, michango imetolewa na Waheshikiwa Wabunge, mingi ikiwa ni ya kujenga. Nasi sote ni mashuhuda kwamba maji ni uhai, tuna uhitaji wa maji na tuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba maji yanawafikia Watanzania wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI ambapo ukienda huko ndiyo unakutana na wananchi ambao wanahitaji maji, hakika tunaamini katika jitihada ambazo zimewekwa na Serikali ya Awamu ya Tano ya kuhakikisha kwamba tunaenda kumtua ndoo mwanamama, ni ahadi ambayo tumeahidi kwa Ilani yetu, nasi tukiahidi huwa tunatekeleza. Kwa hiyo, naamini kwa siku ya leo tuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba tunaunga mkono hoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa zaidi, kuna maneno yamesemwa mengi kwamba kiasi cha fedha ambacho kinatolewa hakitoshi. Ni vizuri pia tukajiridhisha kwamba katika hicho ambacho kinatolewa kiende kikafanye kazi iliyokusudiwa. Kwa sababu haijalishi kiasi cha wingi wa fedha kama management yake isipokuwa nzuri; hakika hata kingekuwa kingi namna gani hakiwezi kufanya kazi iliyokusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni imani yetu na hasa katika utaratibu wa uanzishwaji wa mamlaka ya maji; hapa katikati na wewe ni shuhuda, wakati mwingine ilikuwa tunatupiana mpira, inaonekana hili liko TAMISEMI, hili liko Wizarani, kiasi kwamba sasa ukitaka kufuatilia kujua exactly ni nani ambaye amesababisha wananchi wetu wasipate maji wakati mwingine ilikuwa inatuwia ugumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa utaratibu wetu huu wa kuanzisha mamlaka hii, nawe ni shuhuda, pale ambapo tumeanzisha agency kama TARURA inakuwa ni rahisi kujua exactly nani awe responsible na awe answerable na kila mtu abebe msalaba wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaamini na kwa bahati nzuri sisi kama TAMISEMI tuna utawala mpaka kijjini na kwa sababu Serikali hii ni Serikali moja, kinachofanyika ni kuhakikisha tu kwamba tuna-mainstream ili ijulikane nani anafanya nini, lakini kwa sababu lengo ni kumfikishia mwananchi wa kawaida huduma ya maji, naamini na fedha hizi ambazo zimepatikana na hii agency ndiyo imeanza hivi karibuni, naomba tumuunge mkono Mheshimiwa Waziri na Serikali kwa ujumla na Uongozi wa Wizara ya Maji ili tukasimamie hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu naamini mbele ya safari baada ya hiki ambacho kitakuwa kimetolewa, kikionekana kimesimamiwa vizuri hakijatosha, sasa hoja itakuwa ina mashiko kwamba sasa tuongezee fedha zaidi kwa sababu tuna uhakika juu ya usimamizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami na wewe mwenyewe ni shuhuda, hatuna wasiwasi juu ya uongozi na bahati nzuri kuna mamlaka za maji kila mji. Naamini hakika fedha hii ambayo itaenda kutolewa itaenda kukidhi haja ya kuhakikisha kwamba maji yanapatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe ni shuhuda, wakati fulani ilikuwa ukianza kutafuta fedha unaambiwa nyingine zimeenda Wizara ya Elimu, nyingine zimeenda TAMISEMI, kiasi kwamba unashindwa kuzi-trace kwa ujumla wake, lakini sasa hivi kwa utaratibu huu ambao umeanzishwa hakika Profesa atakuwa na uhakika wa kusimamia kila shilingi na itakuwa ni rahisi kwake yeye kuweza kuwawajibisha wale wote ambao watakuwa hawatimizi malengo ambayo yamekusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hayo machache, naomba niendelee kuunga tena mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa fursa. (Makofi)